The House of Favourite Newspapers

Je, upo katika uhusiano wa aina gani? Kuna dira mbele yako au giza?

Usikubali kuingia mwaka mpya ukiwa kwenye uhusiano wa kupotezeana muda. Ni vema kufanya maamuzi magumu lakini sahihi kwa mustakabali wa mai­sha yako. Usikubali kutumika.

 

Yaangalie maisha katika jicho pana, ukiweka maandalizi mazuri kwa ajili ya kesho yako. Haupo kwa ajili ya kuteswa, kusiman­gwa, kuumizwa moyo nk. Mungu amekuumba maalumu ili ufurahie maisha.

Kamwe mapenzi yasiwe chanzo cha maumivu ya maisha yako ambayo umepewa zawadi na Mungu wako. Marafiki, nina­chosisitiza ni kufanya tathimini na kuanza mwaka mpya ukiwa na fikra mpya.

 

Ok! Sasa hebu turudi kwenye mada yetu ambayo inatufungia mwaka. Wapo wanawake ambao wamekuwa kwenye uhusiano kwa nyakati tofauti na wanaume tofauti na kuishia kuachwa.

 

Marafiki ukweli ni kwamba hakuna kanuni za moja kwa moja kwenye uhusiano, lakini angalau ni vema kuwa na uelewa wa mambo ya msingi zaidi kuyafahamu ili kujipa uhakika wandoa na boy­friend wako.

Wasichana wanaoachwa wen­gi wao hujitathimini sana lakini hawaoni kasoro iliyowaacha­nisha na wapenzi wao ambao awali walikuwa wakitangaza nia ya kuwaoa mara kwa mara.

 

Inawezekana yapo mam­bo mengi zaidi lakini mam­bo haya 7 hapa chini, ukiwa nayo makini, unajisogeza kwenye uhakika wa kuingia kwenye ndoa na boyfriend wako.

KUMKOSOA SANA

Baadhi ya wanawake wana kasumba hii. Boyfriend wake huenda anazungumza jambo au anachangia hoja fulani, yeye an­amkosoa. Mbaya zaidi ukosoaji wake ni ule wa ujuaji, wenye kauli za kutojali na kuonyesha ujuaji zaidi.

Bahati mbaya wanaume kwa namna walivyoumbwa, kihulka hawapo tayari kuwa chini ya wanawake na hawajisikii vizuri kuonekana hawajui. Acha tabia ya kumkosoa mpenzi wako, hata kama una hakika anach­osema siyo sahihi.

 

Lakini kwa uhusiano mzuri, wenye urafiki, zipo njia nzuri za heshima za kumkosoa mpen­zi wako kwa hoja na si kumwon­yesha kuwa ‘yeye siyo lolote’ bali hana elimu au uelewa wa jambo hilo.

Mfano unaweza kumwambia, “Baby lakini ujue unavyosema ni sawa, lakini kwa ninavyojua ni hivi…” kwa lugha nzuri kama hii, mwanaume wako atakuwa tayari kukusikiliza na hutakuwa umemjeruhi hisia zake kwa kumwonyesha kuwa hana uelewa wa mambo.

 

KUMKOSOA MBELE ZA WATU

Kipengele hiki hakina tofauti sana na kilichopita, ila cha msingi hapa ni mbaya zaidi kumkosoa mbele za watu. Njia nzuri zaidi, mwenzi wako ana­pokosea mbele za watu, mpe ishara asiendelee kushikilia hoja yake, kisha baadaye mkiwa wawili unaweza kuzungumza naye kwa utaratibu nilioelekeza kwenye kipengele kilichopita.

 

KUMLINGANISHA NA WA­NAUME WENGINE

Epuka kabisa kumlinganisha mwanaume wako na mwa­naume mwingine. Wapo baadhi ya wanawake wana hulka hiyo. Wanapokuwa kwenye mijadala fulani au kuelekezana kitu kinachohusu majukumu yao, hulinganisha. Ni kosa.

Utamsikia mwanamke anasema, “Jifunze kwa wa­naume wenzako, ona Jumanne anavyofanya kwa mpenzi wake Mayasa.”

Kufanya hivyo ni kumuumiza mpenzi wako, lakini pia kuta­punguza mapenzi na mawazo ya kukuoa. Mwanaume anap­enda kuwa halisi, wa kipekee na asiyelinganishwa na‘mpira wa majaribio’.

Msimamo wako utam­fanya aone anakwenda kumuoamwanamke mwenye heshima, anayejitunza na kuhifadhi maadili.

Kama bado unao usicha­na wako ni vizuri zaidi, lakini hata kama ulishafanya kosa, siyo mbaya kuanza kujilinda kwa upya ili mwisho wa siku, uingie kwenye ndoa ukiwa mpya kabisa kwa mumeo.

Mada yetu itaendelea wiki ijayo ambapo tutamalizia vi­pengele vilivyosalia, USIKOSE!

Joseph Shaluwa ni Mshauri wa Uhusiano anayeandikia Magazeti ya Global Publish­ers. Ameandika vitabu vingi, vikiwemo True Love, Let’s Talk About Love na Maisha ya Ndoa vinavyopatikana kwa oda. Kwa sasa anaandaa kitabu chake kipya cha SIRI ZA NDOA YENYE FURAHA kitakachotoka hivi karibuni.

Comments are closed.