The House of Favourite Newspapers

Jembe la kazi Yanga Lawasili Kambini

0

DIKCSON Job, beki wa kati wa Yanga, jana Jumatano aliwasili kambini baada ya Kocha wa Taifa Stars, Kim Poulsen kumuweka kando katika wachezaji walioenda kupambana na Equatorial Guinea.

 

Habari kutoka kwa mtu wa karibu wa Job, zilieleza kuwa, nyota huyo baada ya kurejea Bongo akitokea Kenya ambapo Taifa Stars ilipiga kambi, kwanza alielekea kwao Morogoro, kisha akaenda kambini.

 

“Job amerejea Tanzania tayari kwa ajili ya majukumu ya timu yake, alipotua alienda Morogoro, kisha leo (jana Jumatano) akaingia kambini walipo wenzake kule Kigamboni,” alisema mtu huyo.

 

Alipotafutwa Job, alisema amerudi Tanzania kwa ajili ya kuendelea na majukumu mengine ya timu yake huku akiweka wazi maendeleo ya majeraha yake.

 

 

“Ni kweli nilipata majeraha madogo wakati wa maandalizi ya mwisho ya mchezo dhidi ya Equatorial Guinea.“Hii ni kutokana na kurejea kutoka majeruhi, hivyo sikuwa sawa, nilishauriwa kupata mapumziko kidogo, lakini kwa sasa naendelea vizuri.

STORI: LUNYAMADZO MLYUKA NA JOEL THOMAS

Leave A Reply