The House of Favourite Newspapers

Jini Mtu-10

0

Niliibuka mbele ya watu wanne katika jumba lililokuwa halijamilika kujengwa, wale watu wanne kimwonekano walikuwa ni vijana waliozamia katika matumizi ya bangi.

Walikuwa wamemdhibiti Nasra kiasi cha haja, mmoja alikuwa amemkwida mikono kwa nguvu huku wawili wakiwa wamemkandamiza kiuno chake sawia kabisa na miguu yake kwa nguvu wakati mmoja alikuwa akifanya mapenzi kwa nguvu na kasi kubwa,.

Nilikuwa nimeibuka nyuma yao, mwili ukinitetemeka kwa hasira iliyo changanyikana na hofu ya kumpoteza Nasra

Jamaa walikuwa wamefanikiwa kufanya mapenzi na Nasra kwa kiwango kikubwa kabisa, na hata yule aliyekuwa akiendelea kumzini alikuwa ni mtu wa tatu baada ya wawili kumaliza haja zao.

“Stoop” nilisema kwa sauti kali,  wale jamaa walistuka mno, walikurupuka kila mmoja na njia yake huku yule jamaaa aliyekuwa akimzini alibaki ameduwaa nyeti kubwa zilizo kuwa wima kama ukuni zilikuwa zikitiririsha mbegu za kiume hovyo.

Na hata nilipo sogea hatua moja mbele ndipo yule jamaa alipo gutuka na kutoka mbio kali, sikuhangaika nao hata mmoja kwani nilijua nitawakamata tu pale nitakapo taka kufanya hivyo,.

Nilimsogelea Nasra na kumwinua alikuwa akilia mno kama mtoto mdogo aliye katwa na wembe katika kidole.

Nilimvalisha vizuri gauni lake, nikampangusa michanga iliyokuwa imemwenea mwili mzima kutokana na kukurukakala za kubakwa.

Nasra aliendelea kulia tena kwa sauti kali, nilitoka nje ya jumba lile na kuangaza mazingira yale ilikuwa maeneo ya kilimahewa, eneo lile halikuwa kabisa na watu lakini pia nyumba zilikuwa  zimeachiana hatua kubwa kutoka nyumba moja hadi nyingine.

Nilitoa mfuko wa Rambo ulio kuwa na chips kavu na maziwa flesh ya tanga katika box dogo.

“Kula chakula hiki”  alinyakua ule mfuko kiwazimu na kukifakamia kile chakula kwa pupa.

Hakulia tena.

  Ndio nisha mkosa huyu mwanamke,atakufa tu siku si nyingi.

Niliwaza moyoni.

Alimaliza chakula chote akawa ameshiba vema, kwakuwa  akili yake ilikuwa fyatu aliendelea na mambo yake ya kiwazimu.

Niliweka tayari kwa ajili ya kumweleza vizuri Nasra juu ya kila kitu kinacho endelea katika maisha yangu na yake huku nikijiapiza kuwa sinto mweleza kama uhai wake upo ukingoni tena na hukana namna ya kumrejesha tena duniani.

Nilimtizama  Nasra akiwa na  sura iliyo onekana kwa macho ya kawaida ya samaki mtu{nguva}, niliongea maneno ya kichawi nikiwa nimekusanyisha mikono yangu pamoja  huku nimeketi kitako kana kwamba nasubiria pilau la hitma na hapo hapo miale kama ya shoti ya umeme ilitokeza katika macho yangu na kumwelekea Nasra..alipiga ukulele wa maumivu na hapo akili ya Nasra ikarejea kuwa sawa.

Alipiga chafya za mfurulizo huku akionekana kama ametoka katika usingizi mzito, alijikagua huku  aking’amua ng’amua macho huku na kule akitizama mazingira ya eneo alilokuwapo.

Kama dakika mbili hivi zilikatika alikuwa yeye akiwa pembeni yangu aligeuza macho na kunitizama katika namna kama kuna mahali aliwahi kuniona kisha akiniita

“Vegasi” niligeuka na kumtizama pasina kuitikia wito wake.

“Tuko wapi huku? na toka lini tuko huku?”

Aliongea kwa sauti yake laini ya upole yenye kutokea puani.

Nilinyoosha mkono wangu kwake ishara ya kumtaka asogee karibu yangu, alishika kiganja changu na kusoge pale nilipo kuwa.

Nilisimama wima huku nikimnyanyua taratubu na kumvuta kifuani kwangu nikamkumbatia  huku nguvu ya pendo nikihisi inanizidia kabisa.

“Nakupenda Nasra, napenda uelewe hilo, leo hadi milele moyo wangu umekufa kwako, siku zote nitapaza sauti yangu kusema neno hilo, labda  siku moja nitakufa mimi, basi nikifa baki ukijua kuwa mwanaume aliyekuwa akikupenda kwa dhati amekufa, pia wewe ukifa nenda ukijua umemwacha mwanaume anaekupenda katika pengo na simanzi kubwa isiyo weza kufutika daima.”

Nilisema huku machozi yakiwa yananitoka donge zito likiwa rohoni mwangu.

Nasra alijichomoa kifuani mwangu akanitizama kwa mkini katika mboni za macho yangu akaendelea kunivulumushia maswali.

“Mwanangu vegasi? Mwanangu yuko wapi”

“Mwanao mzima, yupo nyumbani Nasra”

“Yupo nyumbani? Amebaki na nani?”

Halafu mbona huku panauma.,ume..ume..umeningilia I mean umefanya ngono na mie hivi?” alisema huku akijikagua maungoni mwake,tendo alilo tendewa la kubakwa dakika kumi nyuma akiwa na wazimu tukio lile halikuwepo kabisa akilini mwake.

“Lazma tukae nikueleze kila kitu kinacho tokea Nasra” nilisema nikamshika mkono Nasra na kutoka nae nje ya jengo hilo na kuketi mwisho kabisa wa uwanja wa mpira wa miguu uliotelekezwa kwa kipindi kirefu na kuota nyasi nyingi.

Nilitumia zaidi ya saa nzima kumsimulia kila kitu kilicho tokea katika maisha yangu, sikuficha hata huu uchawi niliokuwa nao mwilini mwangu niliuweka wazi kwa binti huyu. Kitu kimoja tu ambacho sikumwambia  ni juu ya muda wa kuishi alio kuwa nao yeye,.

Nasra alilio mno  alilia  mpaka sauti ikamkauka,  alilia maisha yake yalivyo poteza dira,  alimlilia mtoto wake Husna aliye poteza maisha, kwa hakika aliumia sana, niliona wazi wazi huzuni ya huyu mwanamke iliyo changanyika na  hofu kubwa kabisa,.

Nilitumia zaidi ya masaa mawili mengine kumtuliza Nasra.

“Vegasi”

“Naaam”

“Kwa hiyo wewe hapa uko ndotoni siyo?”

“Ndivyo mpendwa”

“Na pia wewe huyo huyo upo gerezani?”

“Kabisa”

“Halafu ulisema kuwa mimi nilikufa kisha ukafanya nini vile?”

“Nikakufufua upya kwa uhai wa nguva”

Alishusha pumzi ndefu akatizama angani huku amefinya macho yake akionekana kidogo kuwa na mashaka na majibu ya maswali yake katika mengi niliyo yasema eneo hilo kidogo lilimpa tabu kusadiki

“Vile vile ulisema kwamba wewe unaweza kusoma mawazo yangu, na mie pia” aliuliza akionekana kutokuwa na uhakika juu ya hadithi nilizo mpa za maajabu yangu.

“Kila kitu nilicho kwambia ndivyo kilivyo”

“Naona bado hujapona vizuri Vegasi tatizo lako la wazimu halijakwisha kidogo, ila usijali utapona.,Mungu ni muweza”

“Nasra tafadhali, hebu jaribu kuelewa kila kitu nilicho kueleeza” niliongea kwa mahamaniko makubwa.

“Unaweza kuniambia sasa nawaza nini?”

Alinambia huku macho yake yakinitizama kama kwamba ni mwenye kunisikitikia kutokana na kuwa na matatizo ya akili,lakini ndani yake katika haya niliyo mueleza yalileta hisia fulani ya ukweli.

  Ila Mungu ni muweza

Umesema ‘Mungu ni muweza’ nilisema mara moja., Nasra alitoa macho baada ya kuona nimeweza kujua alicho kiwaza akilini mwake alisogea hatua mbili mbali na mimi alinitizama kama ameona maiti ya jini.

Anagalau sasa niliona Nasra anaweza kunisadiki maneno yangu kutokana na kumwonyesha miujiza niliyo kuwa nayo.

“Nasra na siyo hilo tu mpenzi wangu., yapo mengi ambaya huwezi kuamini nakuwa na uwezo nayo, hali hii nimeipandikiza na kwako pia hata wewe unaweza kujua ninacho waza hebu sikia hili ninalo waza kisha uniambie”

Nakupenda

“ Khaa!!. Ndio Vegasi umesema nakupenda nimesikia kitu kama..kama…kama..yanii mithili ya walkman ya Cd kama nimevaa visikilizo vya masikioni..nimeisikia kabisa sauti yako.. sauti yako imesema ‘nakupenda.,uuuwiii Mungu wangu tumepatwa na nini sisi” alipayuka haraka haraka huku akionekana kuchanganyikiwa haswaaa.

Nasra alianza kulia, alipagawa mno hofu ikiwa kuu usoni mwake.

“Nasra” nilimwita huku nikimsogelea.

“Abeee” nahitaji nikupeleke mahali ambapo huwezi ukapata bugudha kutokana jinsi ulivyo”

“Kivipi Vegasi?”

“Kila mtu anajua ulisha kufa sasa ukiingia kwa watu watakushangaa na hata kukuletea zogo”

“No mimi sijafa Vegasi,.naweza nikakuamini katika mengi uliyo yasema lakini siyo la kufa.! nahitaji niende kwa mama yangu na ndugu zangu pia  niwaeleze hili tatizo lakini pia lazma niwatafute maustadh na mashekh kwa ajili ya ufumbuzi wa tatizo hili.”

“Hapana Nasra hakuna binadamu anae weza kusolve tatizo lako,.halafu ni kweli ulisha kufa,. tafadhali Nasra usigome nahisi nafsi yangu inaamshwa huko iliko, natakiwa kurudi kwahiyo kubali upesi nikupeleke eneo salama kwa ajili yako.”

“No…no..noo.Vegasi sitaki.” Alisema Nasra huku akikimbilia vichakani,wakati huo huo nikahisi napatwa na nyenze masikioni mwangu msukomo wa  kuamshwa ukiwa ni mkubwa mno

*******

Nilistuka gafla, nikajikuta nipo katika kitanda cha wagonjwa katika zahanati ndogo ya gereza, nesi alikuwa akiondoa soksi za mikononi baada ya kumaliza kunichoma sindano ambayo kwa kiasi kikubwa iliachangia kuamka katika fahamu zilizo kuwa zimepotea kwa masaa kadhaa.,

“Usipende kuwa jeuli dhidi ya polisi wewe  kijana,watakuja kukungo’o meno siku moja shauli yako.,hawa watu siyo rafiki wa mtu kabisa katika kazi zao”  Aliongea yule nesi mwanamke huku akipanga vifaa vyake vuzuri.

Nilikuwa nimefungwa pingu katika mguu mmoja na mkono mmoja ulio unganishwa na vyuma vya kitanda.

Sikujibu kitu, nilibaki nimelala chali nikitizama katika paa la chumba kile huku mawazo mengi yakipita dhidi ya Nasra.

Nasra uko wapi sasa? nilituma wazo kwa Nasra huko aliko kuwa.

Nilisikia kilio cha Nasra, kilichokuwa katika hali ya woga na wasiwasi mwingi mno.

Nasra tafadhali huna sababu ya kulia hebu nijibu uko wapi sasa

“No no no sitaki..sitaki,..wewe siyo Vegasi wewe,.. ni jini…sitaki.” Nasra alilalama kwa sauti kali, huku nikimsikia akiwa analia mno, kwa hakika huko alikokuwa alikuwa amechanganyikiwa vibaya mno.

   Nasra unaongea nini wewe?

“SITAKIII..” alibwatuka kwa sauti kali ya fadhaa.

Nilikaaa kimya nikijuiliza ni kitu gani nikifanye dhidi ya binti yule.

  Nasra niliita  kwa upole

Kimya.

   Nasra tafadhali usiyongee na mie kwa sauti kwani huko uliko watu watakuona kichaa kwa kuongea peke yako  Nilisema nikituliza fikra zangu kuona ni kitu gani kilikuwa kinapita kichwani mwa yule binti huko aliko.

Fikra za Nasra zilikuwa zimezingilwa na hofu kubwa kabisa huku akiwa hana imani na mimi hata kidogo, aliamini alikuwa amekutana na jini katika maisha yake aliyemtokea kwa kivuli cha Vegasi.

  Sasa Nasra hapo ulipo hebu jitizame uso wako ujione kama ndio wewe ama laa, kisha uniambie huko unako kwenda nani atakaye kusadiki wewe?,.

Nilimtupia wazo kichwani mwake, nikasikia akiguna kisha dakika kama tatu badae nilisika sauti kali ya kupagwa zaidi kwa Nasra, ilikiwa ni baada ya kujitizama katika kioo na kuona ana sura ambayo siyo yake!.

Sura ngeni kabisa machoni pake, japo ilikuwa ni wajihi wenye mvuto mkubwa lakini Nasra alitishika vibaya mno.

Hakuawa yeye aliye jizoea miaka yote alikuwa na sura ya mwanamke mgeni“Unanifanyia nini weweee JINI MTU” alisema Nasra huku akilia na hapo nikasikia watu waliokuwa pembeni yake wakimshanga  yule binti akiongea pake yake huku akilia..

“Nini tatizo ant mbona unaongea mwenyewe huku ukilia?” nilisikia  sauti za watu zilimuhoji.

“Kuna kitu kipo kichwani mwangu,..i mean nina jini..jini mtu linanisumbua kichwani mwangu limebadilisha hadi sura yangu” alisema Nasra lakini kilicho tokea kila mtu alimcheka na kumwona ni mrembo aliye chanyikiwa kwa kiasi kikubwa,.

Umeona sasa Nasra,. hakuna binadamu atakae kuamini,nomba unisikilize mpenzi wangu,.sitaki kukupoteza”

“Nani mpenzi wako wewe shetwani..jini.. nimesema tokaaaaa kichwani mwangu tokaaa”

Alipayuka kwa sauti kali ambayo ilizidi kukusanya watu eneo alilokuwa.kwani nilisikia kila mtu akizungumza lake dhidi ya hali ya Nasra.

Ilibidi nikae kimya nisimsemeshe kabisa ili asiendelee kuonekana  mwehu mbele za watu.

Badae kidogo nilimsikia akihema kwa kasi huku vishindo vya haraka haraka vikisikika, nikajua alikuwa akikimbia, sikujua alikuwa akikimbia kuelekea wapi, lakini alikuwa akikimbia kwa kasi.

Dakika kumi badae,  nilisikia akiita jina la mama yake haraka haraka na hata baadhi ya ndugu zake, nikajua Nasra alikuwa ameeleka nyumbani kwao ambako kulikuwa bado kuna kusanyiko la ndugu zake kutokana na msiba wake kwani mwili wake ulikuwa bado hauja kabidhiwa na serikali kwa ndugu zake kwa ajili ya mazishi..

Nilitega sikio langu vizuri kusikia kile kilicho kuwa kinaendelea kule nyumbani moyo wangu ukiwa na simanzi kubwa kwani tendo lile la Nasra litaleta taharuki kubwa kwa ndugu na jamaa japo hakuna mtu ambaye anaweza kumsadiki moja kwa moja kutokan na sura yake kuwa ya mtu mwingine, sura ngeni kabisa katika macho ya jamaa wanao mjua Nasra.

   Wee binti vipi unamatatizo gani”

   Nahitaji kuonana na mama,.mimi ni Nasra jamani sijafa niko hai nakabiliwa na majini,na mashetani katika kichwa changu,

   Wewe unaonge nini wewe mbona hatukuelewi unacho zungumza. Nilisikia mazungumzo hayo maili nyingi kutoka katika zahanati ya gereza nilikokuwa nimelazwa ni kati ya Nasra na wazee waliokuwa  katika msiba ule huko nyumbani kwao.

   ‘Nasema hivi mimi ni Nasra,sijafa wala sijawahi kufa  nahitaji nimwone mama yangu sasa hvi kwani nina matatizo makubwa’

 ‘Binti naona hauko sawa,labda bange au pombe zinakusumbu kichwani mwako,. kuwa na heshima na tunaomba upotee eneo hili’

‘whaaat,.Mzee hii haiwezi kuwa, mimi nataka kumwona mama yangu sasa hivi’

Alisema Nasra, na baada ya hapo nilisikia zogo kubwa mno kutokea huko alikokuwa makelele ya Nasra akitaka kuonana na mama yake yalitambaa eneo zima huku kila mtu akisema lake kutokana na tukio hilo.

Dakika sita badae kukawa kimyaaa. Sikusikia lolote kutokea huko mtaani,yanii ilikuwa ni kama kwamba nilikuwa nikisikiliza mazungumzo fulani kupitia simu kisha ghafla simu ikakatika mawasiliano.

Hata nilipo jaribu kufutilia fikra zozote katika kichwa cha Nasra kulikuwa kutupu kabisa,

“Nini kimetokea kwa Nasra huko?.

Nilijiuliza lakini hapakuwa na wakunipa majibu. Najua Nasra utakufa laikini siyo leo una siku sita kutokea leo, nahitaji siku hizo sita uone pendo langu, katika siku sita nikufanye mwenye furaha ya mwisho katika ulimwengu, katika siku sita usife ukiwa na donge moyoni mwako, nahitaji tabasamu lako, ufe ukiwa unatabasamu, lakini ni katika hizo hizo siku sita zitatosha kwa kila mtu aliye husika kuhalibu maisha yako na ya mtoto wako yatalipwa kwa kiasi kile kile, ndani ya siku sita za uhai wako.

Nilibaki pale kitandani kwa masaa mawili hadi nilipo kuja kuondolewa baada ya kengele kugongwa ya kufungiwa ndani ya mabweni, ilikuwa yapata saa kumi alasiri.

******

Wafungwa na mahabusu tulifungiwa ndani majira hayo joto la hali ya juu lilikuwa likituadabisha vilivyo katika mabweni yasiyo kuwa  walau mapanga boi.

Nikiwa ndani ya bweni sikuwa na sababu ya kulala majira hayo, kulikuwa na watu walio kuwa wakiendelea na michezo ya hapa na pale kama karata na draft, pia katika kona ya bweni hilo  palikuwa na mlundo wa vitabu mbali mbali katika kikabati kidogo cha mbao, kwa yeyote ambaye angependa kujisomea, ungesogea pale kwa kilanja mtunza vitabu na kuandika jina kisha unachukua kitabu chochote  kwa kujisomea ilimradi kuusogeza usiku kidogo.

Kilanja aliye husika na uangalizi wa vitabu vile alikuwa ni yule mzee shekh Othuman Hilal mwenye hukumu ya miaka ishirini jela.

Nilisogea pale ili walau nipate kitabu kimoja cha riwaya kitakacho  sukuma muda wangu na kuzamia katika njozi inayo nifanya niwe binadamu mwenye uwezo wa ajabu,.

“Vitabu vya riwaya vipo hapa mzee”

“Swadakta,ndio vimejazana humu kama utitiri”

“Nipe kitabu chochote kilicho andikwa na Faraji Katalambula.”

“Jina lako”

“Vegasi”

“Vegasi..? alaa! hivi wewe ndio Vegasi?”

“Ndio mzee” nilijibu, alinitizama huku amekunja uso wake.

“Wewe ndio unakabiliwa na kesi za mauwaji na madawa ya kulevya?”

“Ndio, lakini ni kesi za kubambikiwa”

“Aah! Hiyo siyo hoja mahala hapa kwani  hata akina sisi tuko hapa kwa maslahi ya watu wachache huko uraiani watu kama akini akina Ashim Azizi na kundi lake,. ila ukweli huo anaujua Allah pekee na siyo binadamu..pole sana kijana kesi yako ni ngumu kidogo.

Shekh Othumani Hilal alisema, nilihisi tumbo langu likipata joto vibaya mno kwa kutaja jina la Hashim Azizi kama ni moja ya watu walio sababisha yeye kuwa mahali pale.

Sikumwonyesha mstuko wangu machoni zaidi ya kuifanya sura ionekane ni yenye simanzi kwa ule mtazamo wake kuhusu kesi yangu.

“Ashim Azizi ni nani mzee?”

Nilimuuliza. Lakini shekh Othuman Hilal hakunijbu  moja kwa moja, alikuwa kipekua lundo la vitabu kunitafutia riwaya yoyote ya Faraji Katalambula kama nilivyo taka.

“Unapo mzungumzia Hashim Azizi unamzungumzia mtu mmoja mwenye sura mbili tofauti, kwanza sura yenye huruma,upendo na ari kubwa ya kujitoa kwa ajili ya watu wa tabaka la chini wenye kuhitaji kunyanyuka, lakini pia, sura ya pili ya mtu huyu ni mtu katili mwenye uchu wa pesa, madalaka, mshirikina nambari one, mwenye kuweza kutumia nguvu ya pesa yake na kuipindisha sheria vile atakavyo, huyo ndio Ashim Azizi wengi wakimfahamu kama Saumya kohil” alisema tena yule mzee., tumbo langu lilizidi kupata joto, wakati huo tayari alikuwa amekwisha pata kitabu cha riwaya ya Simu ya Kifo iliyo andikwa na Faraji Katalambula miaka hiyo.

“Kwanini anajiita Ashim Azizi jina la uficho kuliko lile linalo mtambulisha yeye mwenyewe yanii ‘Saumya kohil?” niliuliza tena huku nikipokea kile kitabu cha hadithi.

Lakini wakati  shekh Othumani Hilal ananijibu ghafla nilisikia  sauti katika kichwa changu,alikuwa ni Nasra, ilikuwa ni kama kwamba simu iliyo pigwa eneo fulani kisha ikapokelewa  na zile sauti asilia {natural sound} zikasikika masikioni.

niko wapi hapa? nilisikia sauti ya Nasra ikihoji

Tulia binti uko eneo salama,.naitwa afande Mwita

Haa! Nilishangaa, Kumbe Nasra  alikuwa amepoteza fahamu, kisha alikuwa eneo fulani ambapo bila shaka ilikuwa ni hospitali lakini pia pembeni yake alikuwapo yule askari mwenye lafudhi ya kishashi akifuatilia afya yake pengine hata kufanya nae mahojiano kivipi aibuke kusiko julikana na aende nyumbani kwao Nasra kuliko kuwa na msiba wa Nasra anaye aminika alikufa kwa kupigwa risasi yeye na mtoto wake na maiti yake kuhifadhiwa katika mochwari kabla ya kuibiwa kisha yeye aibuke adai kuwa yeye ndio Nasra!!. ilihali wajihi wake ni tofauti na Nasra anae julikna katika jamii, kwa hakika yule askari makini angehitaji kujua sana juu ya hilo, Moyoni nilimsikitia sana namna anavyo ingia kucheza ngoma asiyo jua maaana yake ni nini.

“Hivi unanisikiliza au uko mbali mwenzetu?”

Alisema shekh Othumani na kunifanya nirudi katika maelezo yake muhimu kabisa.

Lakini wakati huo huo nikasikia yule askari akiuliza jina la  binti aliye kuwa mbele yake.

“Nakusiiliza mzee”

“Hilo siyo jina tu bali ni chama pia,chama ambacho yeye ndiye mwenye kiti wa wafuasi wake,wanatoa kafara za watu,wanakula nyama za watu,mafisadi wa mali za watu, kila aina ya baya chama hiki huwatendea watu,.kwa macho ya juu juu huwezi kung’amua,.  wewe kamsome bwana Katalambula mambo ya Hashim Azizi ni makubwa mwanangu.,”

Alisema yule shekh huku akichukua kitabu kikubwa cha Qurani na kusoma kimya kimya.

Kiasi fulani nilimjua Ashim Azizi, nilijiapiza pale Nasra atakapo fariki basi ndio siku nitakapo anzisha mtiti wa maana dhidi yake, kwani kuna nama fulani nilipatwa na tumaini ya kuwa na nguvu za ajabu.

Niliketi chini na kufungua kurasa za kile kitabu lakini akili yangu ilikuwa maili nyingi kutoka pale nikifuatilia mahojiano kati ya Nasra na afande Mwita.

Kwanini unafanya vurugu katika misiba ya watu binti?

  Sijafanya vurugu mkuu watu wanashindwa kuniamini kutokana na jinsi nilivyo

 Kwani wewe ukoje binti?

  Siko kawaida afande

   Kivipi?

Sura yangu siyo ile ya awali,. labda niseme hivi, nimetokewa na jini lenye kufanana na vegasi na ndiyo kabadilisha kila kitu katika  maisha yangu..

 Wewe Vegasi ni nani kwako?,

  Mchumba wangu

  Unafikili hicho unacho kisema kina sense katika akili za watu makini?”

  Sijui,. lakini ninacho kisema ndicho ninacho maanisha afande.”

  Kwamba wewe ni Nasra na Vegasi ni mchumba wako

  Ndio

  Ningekuwa mimi ndio wewe ningeachana ma matumizi ya bangi na pombe vilevile ningefikilia namna ya kurudi nyumbani kuliko hali hii ya kunga’ang’ania ujinga ambao hauwezi kuingi katika akili za watu makini hata kidogo.

Alisema afande Mwita, kusema ukweli Nasra alizidi kuwa katika wakati mgumu mno, kwani nilisikia akilia wazi wazi kwa uchungu mkubwa.

Ooh mungu wangu hii ni ndoto gani ndefu na mbaya kiasi hiki aagh,.amka Nasra amka  alilalamika mno, mahamaniko yake yalinikumbusha vile na mimi nilivyo kuwa katika ulimwengu wa kutisha wenye kila aina ya unyama, mara zote nilifikili ni ndoto tu, moyo wangu hakuwa tayari kuamini kabisa kama natokewa na matiko yale, niliamini ni moja kati ya ndoto mbaya mno nilizo pata kuota,. lakini ukweli haukubadilika ulibaki kuwa ule.

Nasra alijaribu kuzungumza ukweli wake mwingi wenye kumuhusu yeye, mengi ya ndani aliyasema kwa afande Mwita ili apate kuaminika.

Kulipita ukimya baina yao, kwikwi za kilio cha Nasra ndizo zilizo sikika.

Kila ninavyo jaribu kulichekecha suala lako bado akili yangu inashindwa kukubaliana nalo hata tone.,labda nikushauri jambo moja binti. Alisema afande Mwita, kwikwi zikapungua  ikawa ni sauti za kupandisha kamasi.

Hebu tusubiri hadi majibu ya  daktari, juu ya akili zako ama utendaji wa ubongo wako,kama hutokuwa na tatizo la kiakili,. basi hii issue yako nitaichunguza undani wake ikoje, na kama kutakuwa na mambo ya Kiswahili basi haya watayatatua waswahili wenyewe,.sawa?

  Sawa

Waliagana na afande Mwita akaondoka pale hospitali.

Muda wote nilikuwa nimefunua ukurasa mmoja wa kitabu, hakuna nilicho kuwa nikisoma akili yangu yote ikiwa maili nyingi kutoka mule gerezani.

Sikutaka kumsemesha Nasra katika mtindo ule wa mawazoni  sikuhitaji aendelee kutishika  kwani pia muda si mrefu nilitarajia  kumuibukia kule kule hospitali.

 

Je, nini kitaendelea?
Tukutane Jumatatu asubuhi.

 

 

 

 

 

 

 

Leave A Reply