The House of Favourite Newspapers

Jirani, Kweli We’ Mwanaume Mashine!-8

0

ILIPOISHIA “Si kwa hiki ulichonifanyia, yaani unanikoboa kama vile unahama, kwa mchezo wa leo, najiona siwezi kucheza mechi tena za ugenini kwa wiki kadhaa.” “Mbona leo nimecheza kiwango cha kawaida tu.” “We…! We…! We! “ “Kawaida sana, tena niko na wasiwasi kuwa naweza kufumaniwa na bwana’ako.” “Bwana’angu wa wapi?” “Anayekuweka mjini.” “Mimi napambana na hali yangu bhana.” “Mhh! Haina shida.” Ghafla simu ya Jimmy iliingia ujumbe, akaitoa kwenye suruali yake na kusoma ujumbe uliotumwa. SONGA NAYO… “MPENZI wangu uko wapi? Ujumbe ulikuwa unasomeka hivyo kwenye simu ya Jimmy. Jimmy aliuangalia ule ujumbe wa kwenye simu yake kwa muda kisha akageuka kumuangalia Febo kama anamuangalia, akaanza kujiuliza mara mbilimbili, je, amjibu au ampotezee? “Baby ‘ake, mbona kimya?” Ujumbe mwingine tena ukaingia kwenye simu yake. Jimmy alijiuliza kwa muda mrefu hatimaye aliamua kumjibu aliyemtumia ujumbe. “Niko geto kwangu, nimelala.” “Mmmm! Kulala huko veeepe?” “Kwani nini mpenzi.” Jimmy akajifanya kutuma ujumbe wenye kujibebisha kwa maneno matamu ili anayemjibu asimshitukie kuwa yuko wapi na anafanya nini.
Usikike
“Mbona mimi niko hapa mlangoni kwako.” Jimmy alishikwa na kigugumizi cha muda kwa kuona ameumbuka kwa kusema uongo, hata hivyo aliamua kujikakamua. “Nimelala mpenzi wangu!” “Ungekuwa umelala wala usingeweza kuchati na mimi!.” “Aaah! Kuna kulala na kusinzia, nimelala ila sijasinzia,” Jimmy akajitetea kiaina. “Mmmh! Haya nifungulie basi mlango.” Jimmy akawa kama kapigwa na bumbuwazi asijue nini la kufanya. Alijiuliza kwa muda, wakati huu akili yake ikaanza kutapatapa kutafuta namna ya kujibu jibu lisilokuwa na utata kwa amuulizaye. “Aah…!,” akiwa anataka kumjibu yule mtu wa upande wa pili, ghafla Febo akajivuta hadi upande aliokuwa amelala Jimmy kisha akampandilia juu yake, kama kitoto kidogo kinavyocheza tumboni mwa mama yake. Jambo lililofanya Jimmy aiachie kiaina simu yake. Anna alipoona hajibiwi, aliamua kumpigia Jimmy simu za mfululizo, lakini Jimmy hakupokea. “Mbona hupokei simu.” Febo aliamua kumuuliza Jimmy baada ya kuona simu ile ikiwasumbua mara kwa mara. “Achana naye.” “Kwani ni nani huyo?” “Ni Anna.” “Kumbe huyo, achana naye, ebu tuendelee kula raha zetu.” Jimmy alikubali kwa shingo upande wakati huo Febo alikuwa akivitumia viganja wake kuvipapasa kila idara kwenye mwili wa Jimmy. “Jimmy ninaomba unifungulie mlango mara moja?” Kimya kikapita bila kujibiwa. “Mbona unanitia shaka!” Kimya tena kikapita bila
kujibiwa, Anna anaanza kumpigia simu Jimmy lakini simu yake ikawa inaita bila kupokelewa. “Jimmy mbona unanifanyia kusudi, hivyo au hauko ndani?” Anna akamuuliza Jimmy lakini hata hivyo hakuna alichojibiwa pamoja na kuonekana ujumbe wake wote ulimfikia aliyemtumia. Roho ikaanza kumuuma, maji ya uchungu yakaanza kujikusanya kwenye kimfuko cha kutunzia nyongo na kujitengeneza kuwa nyongo kali. “Najua haumo ndani uliamua kunidanganya, sawa bhana!” Anna aliandika ujumbe wa mwisho ndipo akarudi chumbani na kuendelea na bwana ‘ake. Jimmy alizidi kuhamasika na manjonjo ya mwanamke Febo na kujikuta mkongojo wake ukitamani kunyanyuka upya kwa ajili ya kuanza kutembeza kichapo cha maana kwa awamu nyingine. “Aiiia Jimmmy weeeeeee! “Mh!,” Jimmy aliitika kwa sauti nzito iliyojaa utamu wa tope la mahaba. “Jamani Jimmy, ha..p..o ha..p..oooooo! Shikilia mpenzi wangu, jamani usiachie, sauti nzuri ya Febo ilisikika ikilalamika kwa utamu wa mahaba. Febo alimalizia kwa sauti ya kama anayeumwa sana na anataka kukata roho. Lakini kwa Febo ilikuwa ni sauti yenye kuonesha ushindi kwa kile kilichofanywa na Jimmy, mwanaume mashine ambaye alikuwa hajui kutania anapokutana na mwanamke yeyote ulingoni labda kama awe hujaamua kufanya vyema au awe anaumwa, hana hela au hana mzuka. Jimmy alijizolea ujiko wa maana kwa mwanamke Febo huku chanzo akiwa ni Anna
mwenyewe kuvujisha siri za mapenzi matamu ambayo alikutana nayo kwa Jimmy. “Hakika mapenzi ni kipaji cha hali ya juu, kilichojaa utundu na ufundi wa hali ya juu.” “Kwa nini unasema hivyo?” “Basi tu! Ila…” “Nini tena Febo?” “Si utamu na raha hizi unazonipa?” “Hivi siku zote ndiyo huwa uko hivyo au leo umeniotea tu.” “Nipe nafasi nikuoneshe mziki wake ni kama dude linaloamshwa na wazee wa mjini.” “Basi wewe ni noma sana kwa mtindo huo.” “Mimi naona kawaida tu.” “Siyo kawaida Jimmy, Anna anakila sababu ya kukusifia ingawa sifa zake mbele ya watu waliopinda na wanaozikosa raha kwa wapenzi wao itamkosti sana.” “Kwa nini unasema hivyo.” “Wasifu wako wa ndani nisingeweza kuujua kama siyo Anna kukusifia kuwa uko vizuri kwenye manjonjo.” “Ilikuaje hadi akakuambia hivyo tena.” “Si unajua tena wanawake tukikutana wawili watatu tunakuwa na stori zetu.” “Kwa hiyo mkaanza kusimuliana kuhusu mabwana zenu.” “Siyo hivyo, sema ilitokea tu akaanza kukusifia.” “Ikawaje sasa na wewe ukajitupia kwenye tanuru la moto.” “We’ acha tu, unadhani nani yuko tayari kuona mzinga wa nyuki kwa jirani yake na asiwe tayari kuupakua?” “Mmhh!” “Ndiyo hivyo!” “Kwa hiyo mimi nimekuwa asali au mzinga?” “We’ asali na mzinga kwa sababu unajua kumuandaa mtu
na kumpa dozi ya uhakika hadi akaridhika.” “Huoni kama tumefanya mambo ya ajabu Febo!” “Ajabu yake iko wapi?” “We’ huoni?” “Sioni bhana! Kizuri kula na nduguyo Jimmy.” “Dah!” “Kwani wewe ulikuwa hujui kama Anna ana bwana’ke anayemuweka mjini?” “Mimi simjui ila huwa namsikia tu.” “Hata kama umemsikia, ndiyo anaye sasa.” “We’ acha mapenzi pasua kichwa sana.” Usiku ule ukazidi kuwa mnono kwa Jimmy na Febo kwani safari moja iliwafanya waanzishe safari nyingine na nyingine tena ili mradi ni ujuzi na utundu wa Jimmy ndiyo hasa uliomfanya Febo akanogewa na kujiachia vile atakavyo. Muda wote huo Jimmy hakuwa tena anakumbuka kuhusu ujumbe aliokuwa ametumiwa na Anna ambaye naye akawa chumbani kwake na mwanaume wake. “Samahani mai, nilipitiwa na usingizi? “Niambie!” “Mbona kimya baby!” “Sikielewi jirani.” Jimmy aliendea kutuma ujumbe kwa Anna ingawa hakuwa anajibiwa. Akili yake ikamtuma kuwa atakuwa amelala. Jimmy alimuaga Febo ili aweze kurudi nyumbani kwake. Je, Febo atamkubalia Jimmy aondoke usiku huo kwa raha alizopewa? Je, ujumbe wa Anna ulikuwa unasemaje? Usikose Jumanne ijayo. kwenye gazeti hili. Kwa maoni na ushauri tuma ujumbe mfupi wa maneno (SMS) kwenda namba:+255679979785.

Irene Mwamfupe Ndauka

Leave A Reply