The House of Favourite Newspapers

Tazama Jiwe Kubwa Zaidi Lililopita Karibu na Dunia Jana Jumatano

0

Asteroidi kubwa ambayo inakadiriwa kuwa na ukubwa karibu sawa na wa Jiwe la Gibraltar imepita salama karibu na Dunia.

Asteroidi hiyo ambayo inakadiriwa kuwa na kipenyo cha karibu kilomita 1, ilipita karibu na dunia umbali wa mara tano na umbali kati ya Dunia na Mwezi.

Jiwe hilo ambalo limepewa jina 2014 JO25, ndilo kubwa zaidi kupita karibu na dunia tangu 2004. Wataalamu wa anga za juu walisema fursa nzuri zaidi ya kutazama asteroidi hiyo angani itatokea Jumatano usiku.

Picha za mitambo ya rada zilizopigwa kwa kutumia antena ya Shirika la Anga za Juu la Marekani (Nasa) yenye urefu wa mita 70 (sawa na futi 230) katika kituo chake California zilionesha kwamba jiwe hilo lenye umbo la njugu linazunguka mara moja kila baada ya saa tano.

Asteroidi hiyo iliipita Dunia katika umbali wa kilomita milioni 1.8 (maili 1.1 milioni) saa 13:24 BST, jana Jumatano, Aprili 19.

Inakadiriwa kwamba jiwe jingine kupita karibu na dunia itakuwa mwaka 2027 pale asteroidi ya kipenyo cha karibu mita 800 (nusu maili) iliyopewa jina 1999 AN10 itapita karibu na dunia umbali sawa na wa mwezi kutoka kwa Dunia, takriban 380,000 km (maili 236,000 ).

Leave A Reply