KIKOSI cha Yanga Princess leo kimepoteza kwa kuchapwa mabao 8-1 dhidi ya JKT Queens kwenye mchezo wa Ligi ya Wanawake Tanzania maarufu kama Serengeti Lite Women’s Premier League.
JKT Queens wanafanikiwa kuwafunga watani wote wa jadi baada ya kuanza na Simba Uwanja wa Karume kwa kuifunga bao 1-0 na jana wameendeleza ubabe wao kwa Yanga Princess kwa ushindi wa mabao 8-1.
Yanga Princess wanafanikiwa kuifunga JKT Queens kwani mpaka sasa baada ya kucheza michezo sita walikuwa hawajafungwa bao hata moja.
Alliance Girl walifanikiwa kushinda bao 6-0 dhidi ya Evergreen Queens huku Baobab Queens wameshinda mabao 3-1 dhidi ya Mapinduzi Queens.
Comments are closed.