Johari: Sina Muda na Ray Kwa Sasa Nipo Bize na Kampuni Yangu ya Lokoma
Johari anasema kuwa, yeye na Ray ni zilipendwa na sasa anapambana na maisha yake kwa kushirikiana na mbia wake Chifu ambaye ni Mkurugenzi mwenza katika kampuni yao ya Empire Lokoma.
“Tunazalisha tamthiliya, sasa hivi niko bize na Tamthilia ya Maji ya Shingo inayoruka Azam TV, kuna kazi nyingine nzuri zinakuja hivyo watu wangu wakae mkao wa kula,” anasema Johari.
Johari alikuwa mbia kwenye Kampuni ya RJ na Ray, lakini ilifika wakati wakaachana na sasa kila Mtu anapiga mzigo kivyake.