Vietnam: Waziri wa Mashauri ya Nchi za Kigeni wa Marekani anayemaliza muda wake, John Kerry, amezuru eneo moja nchini Vietnam, ambapo alivamiwa wakati wa Vita vya Vietnam.
Kerry ambaye ni mwanajeshi mwanamaji wa zamani wa Marekani alikutana na mpiganaji wa zamani wa Vietnam, Bwana Tam mwenye umri wa miaka 70 ambaye anakumbuka shambulizi hilo la mwaka 1969 ambapo wawili hao walisalimiana kwa kupeana mikono
Kerry alimuambia hasimu wake huyo wa zamani Vo Ban Tam, kuwa ni vizuri wote wako hai. Bwana Tam ambaye sasa ni mkulima, anasena anafahamu mtu ambaye Kerry alimuua na pia anakumbuka njama yao ya kushambulia mashua ya Marekani.
Bwana Kerry ambaye yuko nchini Vietnam kwa ziara yake ya mwisho kabla ya kuondoka madarakani, alitunukiwa kwa ujasiri wake vitani enzi hizo.
Kerry ambaye wakati huo alikuwa na umri wa miaka 26, alitunukiwa kwa kukinusuru kikosi chake baada ya kumpiga risasi na kumuua mtu ambaye alikuwa akipanga kushambulia mashua yao kwa kombora.