Kiungo na nahodha wa timu ya Simba SC, Jonas Mkude amepata ajali baada ya gari alilokuwa akisafiria na abiria wengine kupinduka katika eneo la Dumila mkoani Morogoro wakati wakirejea jijini Dar es salaam kutokea Dodoma.
Ajali hiyo iliyohusisha gari yenye namba za usajili T 834 BLZ, Toyota VX imetokea baada ya gurudumu la nyuma ya gari hiyo kupasuka na kusababisha majeruhi wawili ambapo wamewahishwa kwenye hospitali ya Mkoa wa Morogoro kwa ajili ya kupatiwa matibabu.