JOSHUA AMCHAKAZA KWA TKO POVETKIN RAUNDI YA SABA (Picha+Video)
MWINGEREZA Anthony Joshua amevunja rekodi ya bondia Povetkin, raia wa Urusi, kwa kumpiga kwa ‘Technical Knock Out’ round ya saba ya pambano kati yao kwenye Uwanja wa Wembley usiku wa kuamkia leo.
Kabla ya bondia Alexander Povektin kupoteza pambano hilo dhidi ya Anthony Joshua kwa TKO, hilo linakuwa pambano lake la pili kupoteza katika mapambano 36 aliyocheza akishinda 34, KO 24 huku Joshua akiendelea na rekodi ya kutopigwa.
Kabla ya pambano hilo Joshua alikuwa akishikilia mataji matatu kati ya manne makuu ulimwenguni katika uzito wa juu (IBF, WBA na WBO) na baada ya ushindi ameongeza taji la IBO World.
JOSHUA | ROUND | POVETKIN |
---|---|---|
9 | 1 | 10 |
10 | 2 | 9 |
9 | 3 | 10 |
10 | 4 | 9 |
9 | 5 | 10 |
9 | 6 | 10 |
56 | TOTAL | 5 |
Comments are closed.