JPM Atoa Maagizo Mazito kwa Watendaji wa Kata Nchini – Video
“Cheo cha ofisa mtendaji wa kata siyo kidogo, ninyi ni wawakilishi wangu ngazi ya kata. Tunapozungumza mafanikio ya Serikali ninyi ndiyo wasimamizi wa mwanzo katika mafanikio hayo.
“Kwa hiyo napenda kuwathibitishia ndugu zangu, tembeeni kifua mbele. Wala kamwe asitokee mtu kuwanyanyasa kule mlipo,” amesema Rais Magufuli.
Kuhusu majukumu ya watendaji hao, Rais Magufuli amesema maofisa hao wana jukumu la kuhakikisha ulinzi na usalama wa kata zao.
Amewataka pia maofisa hao kuwa makini na utoaji wa vitambulisho vya Taifa kwa wageni.
Comments are closed.