JPM, Mama Janeth Wampa Wastara Mil 15/= Za Matibabu (Video)
RAIS John Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli wamechangia Sh. milioni 15 kwa ajili ya matibabu ya msanii Wastara Juma ambazo ziliwazilishwa na Katibu wa Rais, Ngusa Samike nyumbani kwa msanii huyo. Pia aliwasilisha mchango wa Sh. milioni moja na laki tisa kutoka kwa wasaidizi wa Rais.
Global TV ilikuwa ya kwanza kufika nyumbani kwa Wastara na kufanya mahojiano naye ambapo alieleza kwa kina kilichokuwa kinamsumbua na pia alipata fursa ya kuwaomba Watanzania wamchangie ili aweze kupata matibabu ya mguu wake ambao ulikatwa miaka kadhaa kutokana na ajali ya barabarani.
Mahojiano hayo ya katika video ambayo imewekwa chini, baada ya habari hii.
Baada ya hapo, magazeti pendwa ya Global Publishers yaliandika habari hiyo yakiwaomba Watanzania kumchangia msanii na ndipo vyombo vingine vya habari nchini wakiwemo watangazaji wa wa kipindi cha SHILAWADU wakaiendeleza kampeni hiyo ambapo leo Rais John Magufuli na mkewe Mama Janeth wamemchangia msanii huyo.
Global Publishers na vyombo vyake wanatoa rai kwa Watanzania waendelee kumchangia msanii huyo ili aweze kupata matibabu yanayotakiwa.
PICHA/HABARI NA HILALY DAUDI/GPL
Comments are closed.