The House of Favourite Newspapers

JPM: Mbeya Hamkuwa na Mbunge, Mlikuwa na Msanii -Video

0

MGOMBEA urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM, Dkt. John Magufuli, leo Septemba 30, 2020 amewaambia wananchi wa Mbeya kwamba hawakuwa na mbunge wa kuwasemea bali walikuwa na msanii (Joseph Mbilinyi, Sugu), na ambaye si mkali kama kina Diamond na Alikiba.

Ameongeza kuwa vijana wa kiume hupenda kuwa na ‘mshikaji’ wa kike, hivyo amewaomba wananchi hao wamchague mgombea ubunge wa kike atakayewasemea ambaye ni Tulia Ackson.

Aidha, amesema kwa kuwa Jiji la Mbeya lina wilaya moja, ataongeza wilaya nyingine ili ziwe mbili.

MGOMBEA urais (CCM) Dkt John Magufuli, leo Septemba 30, amefanya mkutano wa kampeni jijini Mbeya akiendelea kuomba kura kwa wananchi nchi nzima.

⚫️ Kwa UPDATES zote, Download GLOBAL APP:

⚫️ ANDROID:http://bit.ly/38Lluc8

⚫️ iOS:https://apple.co/38HjiCx

Leave A Reply