The House of Favourite Newspapers

Jumuiya ya Wazazi CCM Kata Azimio Dar, Yatoa Msaada Zahanati Tambukareli

Dar es Salaam, 7 Januari 2023: Jumuiya ya wazazi Kata ya Azimio Temeke, Dar leo imetoa msaada wa vifaa tiba kwenye Zahanati ya Tambuka reli iliyopo kwenye kata hiyo.

Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Kata ya Azimio, Tukae Kondo (kushoto) akizungumza kwenye hafla hiyo.

 

Akizungumza kwenye hafla hiyo Katibu wa Wazazi Kata ya Azamio ambaye ni Kaimu Katibu wa jumuiya hiyo Wilaya ya Temeke, Tukae Kondo amesema kabla ya kutoa msaada huo walitembelea kwenye Zahanati hiyo na kubaini changamoto ya vitanda vya kujifungulia na mengineyo.

Mgeni rasmi Katibu wa Elimu Malezi, Mazingira na Afya mkoa wa Dar es Salaam, Laurian Mganga (kushoto) na Kaimu Katibu wa Wazazi Wilaya ya Temeke, Tukae Kondo (kulia) pamoja na wanachama wote waliohudhuria hafla hiyo hivi ndivyo walivyoanza na zoezi la usafi wa mazingira ya zahanati hiyo.

 

Tukae amesema baada ya kubaini hilo ndipo wameanza na kutatua changamoto hiyo pamoja na vifaa tiba kadhaa walivyotoa kwenye hafla hiyo.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Temeke, Hamis Slim akiwapongeza viongozi wa Kata ya Azimio kwa msaada huo na kuziagiza kata zingine kuiga mfano huo.

 

Tukae amesema huo siyo mwisho wao wa kuisaidia Zahanati hiyo na kusisitiza kuwa huo ni mwanzo tu na wataendelea kuisaidia zahanati hiyo na maeneo mengine kwenye kata hiyo.

Mgeni rasmi kwenye hafla hiyo, Katibu wa Elimu Malezi, Mazingira na Afya mkoa wa Dar es Salaam, Laurian Mganga (kulia) akimpa mkono Mganga Mfawidhi wa Zahanati ya Tambukareli, Zati Haule wakati akimkabidhi msaada huo.

 

Msaada huo ni pamoja na kitanda cha kujifungulia, mashuka, dawa za kufanyia usafi na vitu vingine. Wanachama hao kabla ya kutoa msaada huo walianza na zoezi la kufanya usafi maeneo ya hospitali hiyo na kumalizia na zoezi hilo.  HABARI/ PICHA: RICHARD BUKOS NA ISSA MNALLY /GPL