The House of Favourite Newspapers

JWTZ Lapokea Ndege ya Kijeshi Kutoka Falme za Kiarabu (UAE)

Mnadhimu Mkuu wa JWTZ, Luteni Jenerali, Salum Haji Othman akizungumza kwenye hafla hiyo.

Dar es salaam, 4 Februari 2025: Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mhe. Dk. Stergomena Lawrence Tax (Mb) leo amepokea ndege ya kijeshi  kutoka Jeshi la Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) katika kuimarisha ushirikiano baina ya nchi ya Tanzania na Falme za Kiarabu.

Akizungumza wakati wa mapokezi hayo Dk. ameshukuru na kusema ushirikiano huo uendelee kwa manufaa ya pande zote mbili.

Ndege hiyo ikipewa heshima kwa kumwagiwa maji wakati ikiwasili hapa nchini.

Ameendelea kusema kutokana na kazi kubwa ambayo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan kuona kwamba ushirikiano baina ya nchi hizi mbili unaimarishwa ambapo ndege hiyo itatumika katika shughuli mbalimbali ikiwemo, kusafirisha viongozi mbalimbali wa kiraia na kiserikali, usafirishaji wa kijeshi na kudondosha askari wa miavuli.

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mhe. Dk. Stergomena Lawrence Tax (Mb) akikata utepe kuashiria mapokezi ya ndege hiyo.

“Mashirikiano haya yanayoendelea kati ya jeshi letu na jeshi la Umoja wa Falme za Kiarabu, serikali anayoiongoza rais wetu, Dk.Samia ni kudumisha mahusiano mazuri na nchi rafiki. Jeshi letu lipo tayari kutekeleza majukumu yetu ndani na nje ya nchi na kuhakikisha inakuwa salama”. Alimaliza kusema Waziri Tax. HABARI: NEEMA ADRIAN

PICHA: RICHARD BUKOS /GPL