JWTZ na Jeshi la India Wazindua Mazoezi ya Pamoja Washirikisha Nchi Rafiki 9



Amesema Waziri huyo kuwa kwa sasa changamoto za uhalifu ulimwenguni zinafanana hivyo mafunzo haya ya pamoja yatakuwa na faida kubwa sana kwa nchi zilizoshiriki kwa kubadilisha uzoefu na kuzifanya nchi zetu kuwa salama.

Zoezi hilo litawezesha vikundi shiriki kuongeza ujuzi na uelewa wa pamoja wa kukabiliana na changamoto za kiusalama hasa katika maeneo ya baharini.
Ukiachana na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na India pia zimeshirikishwa nchini tisa zilizopakana na Bahari majeshi nazo yamekuja kushiriki ikiwemo Kenya, Afrika Kusini, Djibouti, Uganda, Tanzania, India, Msumbiji, Madagascar, Comoro, Shelisheli, Mauritius ambazo zimekuja na meli za vita na meli za utawala kwenye mafunzo hayo ya kupambana na matishio baharini.