The House of Favourite Newspapers

Kadja Achanganywa Na Mama Yake

0
Msanii wa Bongo Fleva, Natasha Lisimo ‘Kadja Nito’.

Msanii wa Bongo Fleva, Natasha Lisimo ‘Kadja Nito’ amesema kuwa yupo kwenye wakati mgumu wa kutaka kujifungua huku akiwa bado hajapata na mama yake mzazi.

Akizungumza na Showbiz Xtra, Kadja alisema kuwa anasikitika kuona anatarajia kujifu-ngua wakati hana maele-wano mazuri na mama yake ambaye walito-fautiana baada ya kuamua kuokoka.

“Naumiza sana kichwa nikizaa nitampeleka wapi mwanangu, maana mama hataki kuniona kisa mimi kuokoka. Nachanganyikiwa sijui nikijifungua nimpelekee mjukuu wake amuone au nifanyaje?” Alihoji Kadja.

Leave A Reply