The House of Favourite Newspapers

Kagere + Chama +Luis = Biashara

0

BIASHARA United, leo Alhamisi ina kazi ya kusaka pointi tatu mbele ya Simba ambao ni wageni wao huku rekodi zikionesha kwamba jumla ya mabao ambayo wamefunga timu nzima katika mechi zao za Ligi Kuu Bara msimu huu, hayazidi ya wachezaji watatu wa Simba.

 

Meddie Kagere ametupia mabao tisa, Clatous Chama (6) na Luis Miquissone (2), mastaa hao watatu wa Simba wana jumla ya mabao 17, idadi ya mabao hayo ni moja zaidi ya yaliyofungwa na Biashara United kwenye mechi 19 kupitia nyota wao tisa.

 

Simba itaingia katika mchezo huo utakaochezwa Uwanja wa Karume mkoani Mara ikiwa na rekodi nzuri ya kutopoteza dhidi ya Biashara walipokutana katika michezo mitano.

 

Katika michezo mitano timu hizo zilipokutana, Simba wamefanikiwa kuibuka na ushindi katika michezo minne na kutoa sare mchezo mmoja.

 

Mchezo wa mwisho kukutana kwa timu hizo, ilikuwa Septemba 20, mwaka jana kwenye Uwanja wa Mkapa jijini Dar, Simba iliibuka na ushindi wa mabao 4-0 yakifungwa na Clatous Chama (2) Meddie Kagere (1) na Chris Mugalu (1).

Kwa uchambuzi zaidi wa mechi hii, soma ukurasa wa sita.

WAANDISHI: LUNYAMADZO MLYUKA, MARCO MZUMBE NA MUSA MATEJA

Leave A Reply