The House of Favourite Newspapers

KAHABA KUTOKA CHINA-04

0

Maneno ya Irene kila siku yalikuwa moyoni mwake, moyo wake ukatokea kumuamini Irene kupita mtu yeyote katika dunia hii, hakuona sababu ya kumuamini mtu mwingine zaidi ya msichana huyo ambaye kwake alimuona kuwa zaidi hata ya baba yake. Kila siku alikuwa akiwasiliana naye kwenye simu na kuongea maneno ya kimapenzi huku wakiitana mke na mume.

Walikubaliana katika kila kitu lakini suala la Rose kutumia kiungo cha bandia bado lilionekana kuwa zoezi gumu sana ambalo wala hakuweza kulikubali kutokana na maumivu ambayo aliyoyasikia kila alipojaribu kuutumia kiungo kile.

Siku ziliendelea kukatika mpaka siku ambayo Irene alikuja nyumbani hapo kufikia. Ile kumuona tu, Rose akashindwa kuvumilia, akamfuata na kumkumbatia kwa furaha tukio ambalo lilionyesha ni kwa jinsi gani alikuwa amemkumbuka mtu huyo.

Bwana Shedrack ambaye alikuwa amekuja na Irene ndani ya nyumba hiyo akatabasamu kwa kuona kwamba Rose alikuwa akiufurahia uwepo wa Irene mahali hapo bila kujua kitu kilichokuwa kikiendelea nyuma ya pazia.

Siku ile ikaonekana kuwa furaha kwa Rose, hakuamini kama kweli Irene, msichana ambaye alikuwa akipenda kumuita mume wake alikuwa amefika ndani ya nyumba ile. Kitu cha kwanza mara baada ya kupeleka mizigo chumbani ni kuanza kubadilishana mate kitendo ambacho kiliwachukua muda wa dakika moja nzima.

“Nimekukumbuka mume wangu,” Rose alimwambia Irene ambaye alionekana kuwa mwenye furaha kubwa zaidi.

“Nimekukumbuka pia,” Irene alimwambia Rose na kisha kuanza kupeana mabusu mfululizo.

Siku hiyo walibaki chumbani huku wakiongea mambo mengi. Kwa sababu Irene alikuwa na muda wa wiki moja tu kukaa ndani ya nyumba hiyo kwa ajili ya sikukuu ya Pasaka, akajitahidi sana mpaka anaondoka Rose awe amekwishaanza kuutumia kiungo kile wa bandia ambao alikuwa amemuachia.

Usiku ndiyo muda ambao zoezi lile likaanza kufanyika. Yalikuwa ni maumivu makubwa lakini alitakiwa kuvumilia kwa sababu alikuwa akiingia katika hatua nyingine. Rose alikuwa akipiga kelele za kimahaba huku kifua chake kikiwa juu na huku Irene akijitahidi kumtumikisha Rose kiungo kile cha bandia.

Rose akaanza kufikiria kitu kimoja, tayari alikuwa amekwishaonja raha ya kiungo kile cha bandia ambao alikuwa ameutumia na sasa alijiona kuwa na kila sababu ambazo zilimfanya kutumia kiungo kile ambacho hakikuonekana kama kilikuwa cha bandia wa bandia kwa ajili ya kuona utofauti wake.

Moyoni alikuwa amekubaliana na nafsi yake kwamba ilikuwa ni lazima ajaribu kwa namna yoyote ile kuonja raha ya kiungo ambacho haukuwa wa bandia kama ule ambao alikuwa ameutumia Irene mwilini mwake, kwa kifupi, alikuwa akitamani kufanya mapenzi na mwanaume.

Kitu ambacho alikuwa akikitaka kilikuwa kimoja tu, alitaka kuona ni raha gani ilikuwepo kwa mtu ambaye alikuwa akifanya mapenzi na kiungo ambacho haukuwa wa bandia. Kusagana hakukuisha, mwili wake ulikuwa ukihitaji kusagwa kama msichana ambaye alikuwa akihitaji kufanya mapenzi na mwanaume na Irene alikuwa kwa ajili yake tu.

Usagaji bado ulikuwa ukiendelea kama kawaida. Mawazo ya Rose katika kipindi hiki yakaanza kuhama kabisa, tayari alikwishaona kwamba kulikuwa na kitu tofauti sana mara unapoamua kutumia kiungo cha bandia na ile staili ya usagaji ambayo alikuwa akiifanya Irene mwilini mwake, moyo wake ukabadilika, bado alikuwa akitamani sana kufanya mapenzi na mwanaume ili kuona kulikuwa na kitu gani.

“Mjomba aliniambia kwamba kuna mwanaume anataka kukuoa,” Irene alimwambia Rose.

“Aliniambia pia. Ni mwanaume ambaye alikuwa akinifuatilia toka zamani lakini nikawa simpendi,” Rose alimwambia Irene.

“Kwa nini sasa haumpendi?”

“Basi tu. Sijisikii kuwa na mwanaume katika kipindi hiki,” Rose alimwambia Irene.

“Safi sana. Wanaume ni watu wabaya sana. Wale hawana huruma kabisa, kwanza ukiwapenda sana, wanauumiza moyo wako,” Irene alimwambia Rose.

“Kweli?”

“Ndiyo hivyo.”

“Basi nitaendelea kuwachukia.”

“Hilo ndilo la maana.”

Tayari Irene alikuwa amekwishausoma mchezo, alikwishaona kwamba kama asingeweza kutumia njia nyingine za kumfanya Rose kuwachukia wanaume basi angeweza kumpoteza msichana huyo kwani alikwishaona kwamba aliona raha sana kila akitumiapo kiungo wa bandia alichomkabidhi. Akajiona kutumia nguvu za ziada akilini mwake, nguvu ambazo zingemfanya Rose kuendelea kumuamini yeye na kuachana na wanaume.

“Nitajaribu kufanya mapenzi na mwanaume nione,” Rose alijisemea moyoni.

Wiki moja ikakatika na hatimaye Irene kurudi chuoni. Japokuwa alitamani sana kuondoka na kiungo chake cha bandia lakini Rose akaking’ang’ania na hatimaye kumuachia. Irene hakutamani kabisa kukiacha lakini hakuwa na jinsi, kwa sababu hakutaka kumuona Rose akiwa amekasirika, akaamua kumuachia.

Kazi ikabaki kwa Rose. Kila alipokitumia kiungo kile alikiona kuwa wa tofauti sana kuliko mikono ambayo alikuwa akiitumia Irene katika kuutomasa mwili wake. Kadri siku zilivyozidi kwenda mbele na ndivyo ambavyo hamasa kubwa ya kutamani kuwa na mwanaume ikazidi kumwingia mwilini mwake.

Katika kipindi ambacho Peter alifika nyumbani, mwili wake ulikuwa katika matamanio makubwa sana ila tatizo lilikuwa moja tu, Peter alikuja na gia za kutaka kuwa mke wake. Rose hakuwa tayari, alichokuwa akikihitaji katika kipindi hicho ni kuwa na mwanaume ambaye angefanya naye mapenzi na kumuonjesha ladha tu na si kuwa mume wake wa ndoa kwa sababu bado alikuwa pamoja na Irene.

Hakumkubali Peter kwani aliona kama alikuwa akimzingua. Alichokifanya Rose katika kipindi hicho ni kuchukua simu yake na kisha kuanza kuziangalia meseji ambazo alikuwa ametumiwa na wanaume mbalimbali anaowafahamu na asiowafahamu. Akaanza kuzipitia moja moja mpaka alipotua katika jina la Joshua.

Akaifungua meseji hiyo na kuanza kuisoma. Kama ilivyokuwa kwa wengine, Joshua alikuwa amejielezea vya kutosha kwamba alimpenda na alimuhitaji, alichokifanya ni kumtumia meseji moja tu.

“Nataka kukuona mchana wa leo, tafuta sehemu isiyokuwa mbali na nyumbani, sehemu ambayo tutakuwa wawili tu,” ulisomeka ujumbe huo na kuutuma. Wala haikuchukua muda mrefu, meseji ile ikajibiwa.

“Unataka nionane nawe wapi? Bar au wapi?” meseji hiyo kutoka kwa Peter ilisomeka.

“Huko sitaki. Kuna watu wengi.”

“Basi njoo gheto kwangu, hakuna mtu zaidi yangu.”

“Sawa. Nitakuja saa nane mchana. Naomba uwepo na usimwambie mtu yeyote yule.”

“Usijali. Nitakuwa nakusubiria.” meseji ya Joshua ilisomeka.

Rose akaridhika, tayari alijiona kwamba katika siku hiyo ingekuwa siku maalumu ya kuonja ladha waliyokuwa nayo wanaume katika kufanya mapenzi. Kiungo kile cha bandia kikaonekana kama kumchanganya na kwa sasa alikuwa akitaka kitu chenyewe na wala si cha bandia tena.

Kwake, katika kipindi hicho aliuona muda ukichelewa sana, kila wakati alikuwa akiangalia simu yake ya mkononi, mshale wa sekunde ulikuwa ukichelewa kwenda.

Saa nane kasoro tano mchana Rose akatoka chumbani kwake. Hakutaka kupitia sebuleni kwa kuona kwamba John angemuona, akapitia geti la nyuma na kuondoka. Siku hiyo Rose hakuwa na amani, muda wote macho yake yalikuwa yakiangalia huku na kule.

Alipofika katika sehemu ambayo kulikuwa na nyumba ambayo alikuwa amepanga Joshua, akaanza kuangalia huku na kule, macho yake yakagongana na macho ya Joshua. Mwanaume huyo hakutaka hata kuongea naye, alichokifanya ni kuanza kuelekea ndani ambapo Rose akaanza kumfuata mpaka kuingia chumbani.

“Karibu mgeni,” Joshua alimwambia Rose huku akionekana kuwa na hamu japo kuyaona mapaja ya msichana huyo.

“Asante,” Rose alisema huku akikaa katika kistuli.

“Hicho kibovu. Utaanguka,” Joshua alimwambia Rose huku akitaka akae tu kitandani na wala stuli haikuwa mbovu.

Rose akainuka na kukaa kitandani. Alichokifanya ni kuitoa kanga aliyoivaa na kukibakisha kisketi kifupi ambacho kiliyafanya mapaja yake meupe kuwa nje. Joshua hakutulia, mara alikuwa akifanya hili, mara lile, yaani kila wakati mishemishe hazikuisha chumbani hapo.

Wakabaki wakipiga stori tu. Kitu ambacho alikuwa amekifuata Rose mahali hapo kilikuwa ni kimoja tu, kufanya mapenzi na Joshua ila alikuwa na wasiwasi ni sehemu gani ambapo alitakiwa kuanzia.

Huku akiwaza ni kitu gani alichotakiwa kufanya, kichwa chake kikakumbuka kitu kwamba siku hiyo ilikuwa ni siku ya hatari kwake, siku ambayo kama angefanya mapenzi na mwanaume basi kulikuwa na uwezekano wa kupata ujauzito. Akajikuta akiinuka na kutaka kuondoka.

“Vipi tena?” Joshua alimuuliza Rose.

“Nataka kuondoka nyumbani,” Rose alijibu.

“Yaani umekuja na kukaa kwa dakika kumi tu unataka kuondoka. Usifanye hivyo Rose,” Joshua alimwambia Rose

Joshua akashindwa kuvumilia, kwa jinsi alivyokuwa akiyaangalia mapaja ya Rose pamoja na kifua chake akashindwa kuvumilia. Kama angethubutu kumuacha Rose aondoke ndani ya chumba hicho pasipo kufanya mapenzi lingeonekana kuwa kosa la jinai kwake.

Akamshika Rose mkono na kisha kumkarisha kitandani. Alichokifanya bila kuchelewa ni kuanza kubadilishana mate na kuanza kuupapasa mwili wa Rose. Hapo ndipo utaofauti ukaanza kugundulika kwa Rose. Mikono ya Joshua ilikuwa ni tofauti na Irene, mwanaume, kwake akaonekana kuwa na kitu cha ziada, bila kinyongo chochote kile, akajikuta akimruhusu Joshua aendelee huku kichwa kikiwa kimesahau kama alikuwa katika siku za kupata ujauzito.

“Nakupenda Rose. Nakupenda sana Rose. Nakwenda kufanya mapenzi nawe siku ya kwanza na kuanza mahusiano ya kimapenzi rasmi,” Joshua alimwambia Rose ambaye alimkubalia kwa kutingisha kichwa chake juu na chini.

Rose akafanya mapenzi na mwanaume kwa mara ya kwanza, kila wakati alikuwa akiuona utofauti mkubwa zaidi, raha ambayo alikuwa akiipata ilikuwa ni tofauti na ile ambayo alikuwa akiipata kwa Irene. Walichukua muda wa dakika hamsini, kila mmoja akawa hoi.

“Hivi ulitumia mpira?” Rose alimuuliza Joshua.

“Hapana.”

“Haukutumia?”

“Sikutumia?”

“Kwa nini?”

“Dah! Nilikuwa kwenye presha, nikasahau mpira,” Joshua alijibu.

Rose akashtuka sana, hakuamini kama alikuwa amefanya mapenzi na Joshua bila kutumia kinga. Moyo wake ukaanza kusononeka, hakuamini kama kweli kitendo kile kilikuwa kimechukua nafasi katika maisha yake. Mtu wa kwanza kumfikiria alikuwa baba yake, angemwambia nini endapo angegundua kwamba alikuwa mjauzito, amani ikatoweka moyoni mwake.

“Acha niondoke,” Rose alimwambia Joshua huku akionekana kuwa na haraka.

“Kuna nini tena?”

“Acha niondoke. Tutaongea kwenye simu,” Rose alimwambia Joshua na kisha kuondoka ndani ya chumba hicho.

Mbegu za Joshua zikawa zimeingia katika mayai ya uzazi ya Rose na kuanza hatua zote za kutengeneza kijusi na kisha mtoto kuumbwa ndani ya tumbo lake. Hilo likaonekana kuwa kosa kubwa kwa Rose, kumruhusu Joshua kufanya naye mapenzi ndani ya siku ile ikaonekana kuwa kosa kubwa sana.

Hakujua, hakujua kabisa kama kuruhusu kufanya kitendo kile ndiyo ulikuwa mwanzo wa maisha mapya, maisha ambayo asingeyapenda ila yalikuwa maisha aliyobidi kuyaishi kwa kuwa hakuwa na jinsi wala uamuzi wowote wa kuyakwepa.

****

Uzuri wa Rose uliwateka vijana wengi waliokuwa wakiishi Magomeni Mapipa, kila mvulana aliyebahatika kumuona msichana huyo alitamani kuwa wake kwani alionekana kuwa na mvuto mno. Wanaume hawakutulia, kila siku walimfuatilia msichana huyo ambaye alionekana kumhofia kila mwanaume aliyemfuata.

Watu wakajua kwamba baba yake, Bwana Shedrack ndiye aliyemfanya mrembo huyo kuwa hivyo. Wavulana hawakukoma, kila siku waliweka mitego yao lakini hakukuwa na mtego hata mmoja ambao ulimnasa Rose. Hapo ndipo watu walipoanza kuzitafuta namba zake za simu. Walichokifanya, ni kumtumia msichana Lucy ambaye akajiwekea ukaribu kidogo na Rose na kuchukua namba zake.

Kila mwanaume alizitaka namba hizo huku wengine wakidiriki hata kuzinnunua. Kwa maneno walishindwa hivyo walitaka kumteka kwa kutumia maandishi. Kwa siku, Rose akawa anapokea meseji kutoka kwa wanaume zaidi ya thelathini huku kila mmoja akizielezea hisia zake za kimapenzi kwa msichana huyo ambaye hakuonekana kuwaelewa kabisa.

Kati ya wanaume wote, pia kulikuwa na Joshua, mvulana ambaye kila siku alikuwa akimpenda sana Rose ila hakuwa akipata muda wa kumwambia kwani kila siku Rose alipotoka, alikuwa na wavulana wengine ambao kama walikuwa kwenye mashindano ya kumtaka Rose.

Siku mbili za nyuma kabisa ambazo Joshua alionana na Rose na kuongea naye ndizo siku ambazo wakafahamiana lakini baada ya hapo, hawakuonana tena. Hata siku ambayo Joshua alikuwa akimtumia Rose meseji, Rose alikuwa akimfahamu sana Joshua ambaye alikuwa akijitambulisha lakini katika kipindi hicho hakuwa tayari kuwa na mvulana.

Kila siku Joshua alionekana kuwa mtu wa kuumia tu, kila meseji zake alizokuwa akimtumia Rose hazikuwa zikijibiwa jambo lililomfanya kutokuwa na furaha kabisa. Katika chumba ambacho alikuwa amepanga, usiku kilionekana kuwa kikubwa, kitanda chake alikiona kama kumwagiwa maji kwani kila alipokuwa akijaribu kulala, usingizi haukuja kabisa.

Mawazo juu ya Rose yalikuwa makubwa, kuna wakati mwingine aliatamani kumfuata Rose mpaka nyumbani kwao na kumuulizia lakini ilipofika asubuhi, alikuwa akihofia kufanya hivyo. Vijana ambao mara kwa mara walikuwa wakipewa mkong’oto mbele ya macho yake kutoka kwa Bwana Shedrack walionekana kumuogopesha sana Joshua kiasi ambacho akaamua kutulia huku akiyauguza maumivu yake chumbani kwake.

Mapenzi yakawa mazito moyoni mwake, mapenzi yakamchoma. Hakujua ni kitu gani ambacho alitakiwa kufanya, hakujua ni hatua gani ambayo alitakiwa kuichukua mpaka kuonana na Rose kwa mara nyingine tena na kuendelea kumsisitizia juu ya uamuzi wa kumpenda ambao ulikuwa moyoni mwake.

Mapenzi yalimuuma, mapenzi yalimchoma, kumpenda mtu ambaye wala hakuwa na taarifa na yeye ilionekana kumuumiza sana Joshua kiasi ambacho kila siku alikuwa akiulaumu moyo wake kwa nini ulikuwa ukimpenda sana Rose kupita kawaida. Hakujua ni kwa namna gani angeweza kumpata, ingekuwa anamuona nje ya nyumba yao akiwa peke yake ingekuwa afadhali, ila tatizo lilikuwa moja tu, kila alipokuwa akitoka, wasindikizaji walikuwa wengi.

Joshua akakata tamaa, hakujua ni kitu gani ambacho alitakiwa kukifanya kwa wakati huo. Kama kupenda alikuwa amependa sana na wakati huo moyo wake ukaonekana kama kukata tamaa. Maneno juu ya uzuri wa Rose bado yalikuwa yakiendelea kusikika kama kawaida lakini hakutaka kumwambia mtu yeyote kwamba na yeye pia alikuwa mmoja wa wafuatiliaji wazuri wa Rose.

Katika siku hii ya leo, Joshua hakutaka kufanya jambo lolote lile, kwa kuwa alikuwa amechoka, hata kufuatilia biashara zake akapuuzia na kisha kukaa tu nyumbani. Siku hiyo ndio alichukua muda mrefu sana kumfikiria Rose ambaye kwake alionekana kuwa kama malaika mzuri aliyeshushwa kutoka Mbinguni. Huku akiwa katika hali hiyo, mara meseji ikaingia. Hakutaka kupoteza muda, hapo hapo akaichukua simu yake na kuufungua ujumbe huo.

Kwanza akashtuka pale kitandani alipokuwa amelala, akainuka na kisha kukaa kitako. Akayafikicha macho yake na kisha kuuangalia vizuri ujumbe ule, ulikuwa ni ujumbe ambao ulitoka kwa Rose. Bila kuchelewa, bila kuuliza kwamba ilikuwaje, akaujibu.

Siku hiyo ndio ambayo Joshua akafanya mapenzi na msichana Rose na kisha kuziruhusu mbegu zake kuingia katika mfuko wa uzazi wa Rose na hatimae kuanza kutengeneza kijusi.

 

Je, nini kitaendelea?

Tukutane kesho hapahapa.

Leave A Reply