KAJALA SASA AUCHUKIA MWILI WAKE
MREMBO kutoka Bongo Movies, Kajala Masanja amefunguka kuwa kati ya vitu ambavyo anavichukia kwa sasa ni pamoja na mwili wake kuwa mnene kupitiliza.
Ame-sema ubonge wake kwa sasa umefikia kiasi cha kumnyima raha kwani hata nguo zake nyingi ameshi-ndwa kuzivaa kwa sababu hazimpiti mwilini.
“Jamani huu mwili mpaka nahofia naweza kupata presha au gonjwa lolote linalotokana na kunenepa sana maana hata mazoezi naona sasa yamedunda, najitahidi kupambana ili niweze kurudi kama zamani,” alisema.
Comments are closed.