The House of Favourite Newspapers

Kajala yupo tayari kuuza kila kitu, kisa Paula

STAA wa filamu za Kibongo, Kajala Masanja amesema kuwa atamsomesha mtoto wake, Paula Paul hadi mwenyewe aseme basi na hata kama akiishiwa hela, yupo tayari kuuza kila kitu ilimradi bintiye huyo asome.  Akizungumza na Amani, Kajala alisema, kitu ambacho anakizingatia kwa mtoto wake huyo ni kusoma bila kuchoka kwa sababu yeye hakusoma ipasavyo.

“Unajua ukiwa hujapata fursa ya kusoma ipasavyo, unapokuwa mkubwa ndiyo unagundua maana halisi ya kusoma. Sasa kwa vile mimi sijasoma kivile, napigana mtoto wangu asome kwa namna yoyote, hata vitu vyangu vya ndani nitauza,” alisema Kajala bila kutaja elimu yake.

Stori: Imelda Mtema

Comments are closed.