Kamati Kuu CCM yapitisha majina 3 ya Uspika
KAMATI Kuu ya Chama Cha Mapinduzi leo imewapitisha Ndugu Job Ndugai, Ndugu Abdullah Ali Mwinyi na Dk. Tulia Ackson Mwansasu kugombea nafasi ya Uspika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kikao cha kupitisha majina hayo kimefanyika katika ukumbi wa makao makuu ya chama hicho mkoani Dodoma kikiongozwa na Mwenyekiti wake ambaye ni Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Dk. Jakaya Kikwete.