The House of Favourite Newspapers

Kamati Kuu ya CCM Yapitsha Majina ya Wagombea Nafasi Mbalimbali

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, akiongoza kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC), tarehe 10 Machi 2025, jijini Dodoma.

Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), chini ya Mwenyekiti wake na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, imekutana Machi 10, 2025, Jijini Dodoma ambapo pamoja na mambo mengine imepitisha majina ya Wagombea wa nafasi mbalimbali za uongozi zilizokuwa wazi ndani ya CCM na Jumuiya zake kwa nafasi za Wilaya na Mikoa.