The House of Favourite Newspapers

Kamwaga Amuomba Radhi Samatta

0

Aliyekuwa Kaimu Afisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga amemuomba nahodha wa timu ya Taifa Stars, Mbwana Samatta kutoa msamaha kwa watu wanaombeza na kumtwisha mzigo wa lawama pindi timu hiyo inapofanya fanya vibaya.

 

Kupitia ukurasa wake wa Twitter Kamwaga amesema watu wengi wamekuwa wakimtupia lawama Samatta pindi timu inapofanya vibaya tu lakini inapofanya vizuri wanawapa sifa watu wengine.

 

“Utusamehe sisi Watanzania kwa kukubebesha mzigo mzito. Kila timu ikifanya vibaya, zigo la lawama lote kwako. Ikifanya vizuri, sifa kwa wengine” ameandika Kamwaga katika ukurasa wake wa Twitter.

 

Kamwaga amesema “Wakati wa kukusifu na kuimba jina lako utafika. Ulitupeleka AFCON na sasa kuna ndoto nyingine kubwa zaidi. Ahsante sana” amesema Kamwaga.

 

Taifa Stars jana ilishinda bao 1-0 dhidi ya Benin katika mchezo wa kufuzu Kombe la Dunia nchini Qatar 2022.

 

Leave A Reply