Camerlengo Farrell Aongoza Ibada Ya Kufunika Mwili Wa Papa Francisko, Kuzikwa Leo -Live Update Video
Aprili 25, 2025 Camerlengo, Kardinali Kevin Joseph Farrell, Askofu Mkuu Diego Ravelli waliongoza Ibada ya kufunika mwili wa Baba Mtakatifu Francisko na mwisho alisoma hati ambayo iliwekwa kwenye jeneza.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka idhaa ya kiswahili ya Radio Vatican, Misa ya Mazishi itaanza saa 5:00 kwa saa za Tanzania leo Aprili 26, 2025, katika Uwanja wa Mtakatifu Petro mjini Vatican.