The House of Favourite Newspapers

Kaze Aahidi Makubwa Yanga

0

AKITARAJIWA kutua leo Alhamisi saa 4 usiku, kocha mkuu mpya wa Yanga, Mrundi, Cedric Kaze, amewatumia ujumbe mkubwa mashabiki wa timu hiyo akiwaambia kwa pamoja watafanya makubwa.

Kauli hiyo aliitoa kocha huyo akiwa njiani kutua hapa nchini akitokea Canada ambapo makazi yake yalikuwa huko.

Kocha huyo anakuja kuifundisha timu hiyo baada ya kufikia makubaliano mazuri na mabosi wa Yanga akichukua nafasi ya Mserbia, Zlatko Krmpotic aliyetimuliwa hivi karibuni.

“Ninajivunia kuwa kocha mpya wa Yanga, timu yenye historia nzuri ambayo mashabiki wake ni wazuri.“Yanga ni kati ya timu bora katika Ukanda wa Afrika, kwa pamoja tutafanya makubwa,” alisema Kaze.

 

Kaze atatua leo na moja kwa moja atajiunga na kambi ya Yanga iliyowekwa kwenye Kijiji cha Avic Town, Kigamboni nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam tayari kwa ajili ya kuanza kibarua cha kukinoa kikosi hicho.

WILBERT MOLANDI, Dar |SPOTI XTRA

Leave A Reply