The House of Favourite Newspapers

Kejeli za kutopata mtoto… Mchungaji Akesha Akimwombea Wema

0

wemaWema Isaac Sepetu ‘Madam’

Stori: Gladnes Mallya, Ijumaa

Dar es Salaam: Habari njema! Baada ya staa wa filamu za Kibongo, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ kupewa kejeli nyingi za kutopata mtoto akipachikwa majina ‘negativu’ ikiwemo mgumba, mchungaji aliyetambulika kwa jina la Daudi Mashimo amepata maono juu ya mlimbwende huyo na kuamua kukesha akimuombea apate mimba.

NI WA KIUME KAMA SAMWELI

Akizungumza na Gazeti la Ijumaa mapema wiki hii, mchungaji huyo anayeongoza kondoo katika Huduma ya Injili ya Maumivu na Uponyaji iliyopo Mbezi-Msakuzi jijini Dar, alisema kuwa akiwa kwenye maombi nyumbani kwake, siku moja majira ya mchana, alipata maono kutoka kwa Mungu kwamba, ndani ya mwaka huu lazima Wema azae mtoto wa kiume.

 mchungaji (2) Mchungaji Mashimo.

Mchungaji Mashimo alisema kuwa, katika maono hayo, alioneshwa kwamba, mtoto huyo atakuwa ni wa kipekee kwani atakuwa mtoto wa agano kama ilivyokuwa kwa Samweli wa kwenye Biblia.

SIKU SABA ZA NAOMBI

Alifunguka kwamba, baada ya maono hayo aliwashirikisha watumishi na baadhi ya waumini wake hivyo wale waliokubaliana na maono hayo walitenga siku saba ambapo walikuwa wakimuombea Wema usiku na mchana ili Mungu ampe mtoto kama maono yalivyoonesha.

mchungaji (1)“Wema amekejeliwa na kudhihakiwa sana, sasa kupitia yeye Mungu anataka afanye muujiza, atampatia mtoto na Mungu hasemi tu mtoto bali ni mtoto wa kiume, yaani atakuwa Samweli wa pili, iwe ameolewa au hajaolewa, haijalishi. Ila ni kwamba Mungu amenionesha hivyo.

“Tumekuwa na maombi ya siku saba ya usiku na mchana hapa kanisani (Mbezi-Msakuzi), tukimuombea Wema ili apate mtoto kama Mungu alivyonionesha na naamini hilo linakwenda kutimia ili Watanzania wapate sababu ya kumtukuza Mungu kupitia mwanadada huyo kwani Mungu amesikia kilio chake,” alisema Mchungaji Mashimo.

USHUHUDA KWA TAIFA LA TZ

Mtumishi huyo alisema, kusudi la Mungu kumpa maono hayo ni kubwa kwani Wema amekuwa akidharauliwa kwamba hazai hivyo haijalishi ni mchafu kiasi gani ila Mungu atajiinua kwake ili watu waamini kuwa yupo na hakuna linalomshinda kwa sababu mtoto wa kiume atakayezaliwa atakuwa wa ushuhuda kwa Taifa la Tanzania.

WEMA: IPO SIKU NITAITWA MAMA

Jitihada za kupata Wema kuzungumzia maombi hayo yanayofanywa na mchungaji huyo kwa kushirikiana na waumini wake hazikuzaa matunda ila kuhusu suala hilo la kupata mtoto, Miss Tanzania huyo wa mwaka 2006/07 hivi karibuni alisema kuwa, watu wamekuwa wakizungumzia ishu hiyo lakini anamuachia Mungu akiamini kuwa, ipo siku naye ataitwa mama.

TUJIKUMBUSHE

Wema amekuwa akipewa maneno mabaya ya kejeli kutoka kwa watu mbalimbali kwamba hazai na hii ni baada ya yeye mwenyewe kuwahi kukiri kuwa hawezi kuzaa kufuatia vipimo alivyofanyiwa na daktari wake.

Hata hivyo, miezi kadhaa iliyopita alikiri kuwa na ujauzito wa mpenzi wake wa sasa, Idris Sultan ambao baadaye ulichoropoka.

Katika sekeseke la Wema kutopata mtoto, hivi karibuni, chipukizi wa Bongo Fleva, Rajabu Abdulhan ‘Harmonize’ alidaiwa kumkejeli Wema kwa kusema kuwa hazai, jambo lililomchukiza hata mama mzazi wa Wema, Mariam Sepetu ambaye aliwaka akisema kuwa watu waache kumwandama mwanaye huyo.

Leave A Reply