The House of Favourite Newspapers

Kessy kampa kampa Ngoma

0

NGOMA AKISHANGILIA GOLI (5)Ngoma na Bosou

KOCHA wa Yanga, Hans van Der Pluijm, amesema ana matumaini na ameomba timu yake isifanye makosa katika mchezo wa kesho Jumapili dhidi ya MO Bejaia kwenye Uwanja wa l’Unite Maghrebine jijini hapa.

Yanga inacheza na MO Bejaia mechi yake ya kwanza ya Kundi A kuwania Kombe la Shirikisho Afrika na Pluijm raia wa Uholanzi ana matumaini ya ushindi kwa kikosi chake.

Jambo linalosubiriwa kwa hamu na mashabiki wa Yanga ni kuona beki wao mpya Hassan Kessy akiichezea timu hiyo kwa mara ya kwanza akitokea Simba.

KessyKessy

Katika mechi dhidi ya Yanga, Machi 20, mwaka huu, Kessy akiichezea Simba alipiga pasi fupi iliyowahiwa na straika Donald Ngoma (Yanga) kisha akafunga na kuzua mjadala wa Kampa Kampa Ngoma.

Pluijm ana nafasi kubwa ya kumtumia Kessy katika beki ya kulia ili kuziba nafasi ya Juma Abdul anayesumbuliwa na maumivu ya enka, pia beki wa kati na nahodha Nadir Haroub ‘Cannavaro’ hayupo kikosini akitumikia adhabu ya kadi nyekundu.

“Baada ya kambi yetu ya Uturuki, tutaona tulichopata, sitaki kumpa presha mchezaji yeyote yule. Soka ni mchezo wa makosa, yeyote anaweza kufanya kosa na akajutia.

“Tunawajua wapinzani wetu na kuna sehemu muhimu wapo makini na tayari tumezifanyia kazi, tuingie uwanjani na matumaini ila hatutaki kufanya makosa,” alisema Pluijm, raia wa Uholanzi.

Katika mchezo wa kesho utakaochezeshwa na mwamuzi Bouchaib El Ahrach raia wa Morocco, Pluijm anaweza kumtumia beki wa kati Andrew Vincent ‘Dante’ katika nafasi ya Cannavaro akicheza sambamba na Kelvin Yondani kwani Vincent Bossou anayetumika mara kadhaa, amefanya mazoezi siku chache baada ya kuchelewa kujiunga na kambi ya Uturuki.

Yanga iliyoingia kambini Uturuki Jumapili iliyopita, iliondoka nchini humo kuelekea Algeria ambako ilifika jana saa 7:00 mchana tayari kwa mechi ya kesho. Yanga inatarajiwa kupangwa hivi: Deo Munishi ‘Dida’, Kessy, Oscar Joshua, Dante, Yondani, Thabani Kamusoko, Simon Msuva, Haruna Niyonzima, Ngoma, Amissi Tambwe na Deus Kaseke.

Katika mchezo mwingine wa Kundi A kesho, TP Mazembe ya DR Congo itacheza na Medeama ya Ghana kwenye Uwanja wa TP Mazembe, Lubumbashi, DR Congo.

Leave A Reply