The House of Favourite Newspapers

Kiburi cha Costa na Jeuri ya Chelsea

0

 

Die­go Costa.

SAKATA la Die­go Costa kugoma kurejea Chelsea bado li­nashika kasi na kuwa gum­zo duniani kote. Straika huyo yupo nchini Brazil ak­iendelea kupumzika wakati wachezaji wenzake wa Chelsea wakiendelea kucheza mechi za Premier. Mhispaniola huyo mwenye asili ya Brazil, kagoma kure­jea Chelsea kwa kuwa hana maele­wano na kocha wake Muitaliano, Antonio Con­te.

Uhusi­ano wake na Conte ulizo­rota muda mfupi baada ya msimu kuisha, kuto­kana na raia huyo wa Italia kumueleza kuwa hayupo kwenye mipa­ngo yake ya msimu ujao, hivyo kum­taka atafute timu. Kuanzia hapo hadi leo, Costa amego­ma kufanya kazi katika kikosi cha Chelsea kilicho chini ya Conte.

Unapo­tazama saka­ta kama hili ni lazima ujiulize maswali mengi, hasa kama ukiwa ni mtu wa kuta­fakari mambo. Conte ameshasema Costa hayupo kwenye mip­ango yake na tayari amesham­leta Alvaro Morata kutoka Real Madrid kwa ajili ya kuziba pen­go lake, kwa hiyo busara hapo ni kumuuza tu Costa.

 

Atletico Madrid inamtaka Costa, 28, kwa dau la zaidi ya pauni milioni 35 ambazo Chel­sea ilizitoa ili kumnasa miaka mitatu iliyopita, lakini straika huyo pia naye anataka kutimkia klabuni hapo. Sikiliza vizuri hoja ya Costa. Anasema: “Hatima yangu tayari nil­ishaiamua. Lazima nirudi Atletico Madrid. Kikwazo kikubwa kinachobaki ni kwamba Chelsea haitaki kuniachia.

“Niliwaambia kwamba kama sipo kwenye mipango yao, ningependa niamue hatima yangu mwenyewe. Sitawaruhusu waamue tu ili watengeneze pesa zaidi.

Die­go Costa.

“Nilipokuja Chelsea wal­ilipa pesa kidogo kuliko ambayo Atletico wanataka kuitoa sasa. Nadhani wa­napaswa kuzingatia kila nili­chowafanyia. Siyo kosa langu kwamba sipo klabuni hapo. Kama lingekuwa ni suala langu ningekuwa nacheza.

 

“Sasa ni mwezi mzima. Ma­pumziko ni mazuri lakini yakizidi yanachosha.”

Unachoweza kujiuliza hapo ni kuwa kama Chelsea imesha­tangaza kuwa haina mpango naye msimu huu, Atletico Madrid ipo tayari kumnunua na yeye anataka kuondoka, kwa nini basi Chelsea haitaki kumuuza?

Kama imeshaleta hadi strai­ ka mbadala, kwa nini haitaki kumuachia? Kwa nini inataka kumuuza kwa bei kubwa zaidi ya ili­vyomnunulia wakati alitua hapo akiwa tayari ni staa, akawa­fanyia mambo, na sasa umri wake umesogea?

 

Fikiria kile ambacho Cos­ta ameifanyia Chelsea tangu alipotua hapo mwaka 2014 kwa dau la pauni milioni 32 akitokea Atletico Madrid, halafu fikiria pia jinsi inavyotaka kuachana naye.

Nikukumbushe kidogo tu kuwa kwa misimu mitatu ambayo Costa amecheza Chelsea, mara zote amekuwa mfungaji bora klabuni hapo huku akifanikiwa kuipatia ubingwa wa Premier mara mbili (2014-15 na 2016-17).

Ninakubali kwamba Costa ana ka­sumba ya utukutu, ni jeuri na kiburi kwelikweli, lakini kwa kujitoa kwake huko kwa nini Chelsea isingetumia busara ya kuachana naye kwa amani?

Kuna faida gani ya kuendelea kumng’ang’ania mchezaji ambaye wamemu­eleza kuwa hawamtaki na kumtaka atafute timu?

Conte.

Kama walitaka aendelee kuichezea Chelsea, kwa nini sasa Conte alimtumia meseji na kum­wambia hayupo kwenye mipango yake na kumtaka atafute timu?

Sasa sakata lao limefikia pabaya, kwa kuwa tayari Chelsea imeshaanza kumka­ta mshahara kutokana na kutokuoneka­na klabuni, na imetishia kuwa itakuwa ikimkata kiasi cha pauni 300,000 (zaidi ya Sh 854m) kwenye mshahara wake, kila baada ya wiki mbili asizoonekana, hatua ambayo imesababisha Costa atafute wanasheria wa kumsaidia, kwa kuwa kiburi chake ni kwamba katu hawezi kuru­di kuichezea Chelsea kwa kuwa ameshaambiwa hatakiwi na atafute timu.

 

Wiki moja iliyopita, Costa alilalama kuwa Chel­sea inamnyanyasa na inamtendea kama mny­ama. Alisema: “Ninaisubiri Chelsea iniweke huru. Kwa nini hawataki niondoke kama hawanitaki?

“Uamuzi wangu ni kwenda Atletico. Nimes­hazungumza na mkurugenzi wa Chelsea, Marina Granovskaia. Nilisema ‘kama kocha hanitaki, na­taka niende Atletico Madrid’.

“Wanataka niende kule nifanye mazoezi na kikosi cha watoto. Sitakuwa naruhusiwa kuin­gia kwenye vyumba vya wachezaji wa kikosi cha kwanza na sitakuwa na mawasiliano kabisa na washkaji. Mimi siyo mhalifu! Sidhani kama ni haki kunitendea hivi baada ya yote niliyowafanyia.”

 

Mantiki ya kumwambia afanye mazoezi na kikosi cha kwanza ni ipi?

Najua kwamba Chel­sea inataka Costa afuate uta­ratibu kwa kure­jea klabu­ni, laki­ni kama aliambiwa atafute timu wakati akiwa mapumzikoni, arudi kufanya nini kama timu ime­shapatikana? Wana­chotakiwa ni kumua­cha aondoke zake kwa amani tu.

Watumie busara na kutambua mchan­go wake na namna ya kuachana naye, waachane na kiburi chake ambacho kocha wake wa zamani, Diego Simeone ndiye anayekiweza.

 

Hata hivyo, Costa hataweza kuichezea Atleti­co mpaka mwakani, kwa kuwa klabu hiyo ina adhabu ya kutosajili hadi Januari.

Kitu ambacho kinaweza kufanyi­ka ni kwa Costa kwenda kwa mkopo kwa Wahispaniola wengine, Depor­tivo La Coruna mpaka Januari.

Kingine kinachoweza kufanyika ni kujiunga na Atletico Madrid sasa lakini akae miezi michache akifanya mazoezi peke yake bila kuichezea timu hiyo hadi Januari. Hayo yote anayataka lakini siyo kubaki Chelsea.

MWANDISHI WETU, Dar es Salaam

 

Usipitwe na Matukio, Install ===>Global Publishers App

Sikiliza Hadithi za Mtunzi Eric Shigongo Hapa

Leave A Reply