The House of Favourite Newspapers

Kidoa: Nilibanwa Sana, Sasa Napumua

0
Muuza nyago kwenye video za Bongo Fleva ambaye pia ni msanii wa filamu, Kidoa Salum

 

MUUZA nyago kwenye video za Bongo Fleva ambaye pia ni msanii wa filamu, Kidoa Salum amesema kuwa mwanzoni mchumba wake (jina kapuni) alikuwa akimbana kila kona lakini kwa sasa anapumua kwa kuwa amekuwa muelewa.

 

Akizungumza na Star Mix, Kidoa alisema kuwa, mpenzi wake alikuwa hamuelewi kabisa kuhusiana na kazi zake za kuuza nyago na filamu lakini walivyokaa kwa muda ameweza kumjua na kumuamini.

“Jamani zamani naona hata watu walikuwa hawanielewi kabisa lakini mpenzi wangu ndio alikuwa hataki nitoketoke au kujikita zaidi katika mambo ya sanaa lakini nashukuru Mungu sasa hivi ameniachia uhuru na ninafanya hata Tamthilia ya Huba,” alisema Kidoa.

Umeona Kilichotokea Kwenye Birthday Ya Wema? Tazama Hapa

Leave A Reply