The House of Favourite Newspapers

Kigogo Usalama Anaswa kwa Dawa za Kulevya – Video

Naibu Kamishna James Lukas akizungumza mbele ya wanahabari hawapo pichani.

 

MAMLAKA ya kudhibiti na kupambana na dawa za kulevya nchini inamshikilia aliyekuwa Afisa Usalama wa Shirika la Posta nchini, George Mwamgabe,  kwa tuhuma za kujihusisha na usafirishaji wa dawa za kulevya.

George Mwamgabe, alipoonyeshwa mbele ya wanabahari.

Akizungumza na wanahabari makao makuu ya mamlaka hiyo jijini Dar es Salaam, Kaimu Kamishna,  James Lukas, amesema afisa huyo na wenzake walikamatwa kwenye oparesheni maalum iliyofanyika kipindi cha mwezi huu wa Septemba.

Kamishna wa Huduma za Sheria, Edwin Kakolaki, akichambua mambo ya kisheria.

Kamishna James amesema afisa huyo alikuwa akishirikiana na wasafirishaji wa madawa hayo ambapo akiwa katika mahojiano alitoroka mpaka alipokamatwa wiki iliyopita.

Makamishna wa mamlaka hiyo wakati mkutano ukiendelea.

Katika mkutano huo kamisha huyo na viongozi wenzake walimuonyesha afisa huyo na wenzake waliokamatwa na madawa hayo sehemu mbalimbali Dar es Salaamna Mwanza.

Wengine waliokamatwa kwenye oparesheni hiyo ni pamoja na Hassan Azizi, Hassan Shaban, William Sebastian, Hamdan Mwakilonga na Felix Odemba.

Watuhumiwa wakiwa na mifuko yenye dawa za kulevya aina ya heroini waliyokamatwa nayo.

 

Kamishna huyo aliyataja madawa hayo kuwa ni heroini zaidi ya kilo moja na mirungi kilo 214.

Wakati akisema hayo alitoa tahadhari kwa wote wanaojihusisha na biashara hiyo na kuwaambia kwamba serikali inayoongozwa na Rais John Magufuli iko makini katika kuwadhibiti na yeyote atakayeendelea kufanya biashara hiyo ataishia pabaya.

Wanahabari wakiwa kazini leo.

 

HABARI/PICHA: RICHARD BUKOS /GPL    

 

Comments are closed.