Kijana wa Miaka 24 Agombea Urais Uganda
KIJANA John Katumba ameandika historia nchini Uganda kuwa mgombea urais binafsi mwenye umri mdogo akiwa na miaka 24.
Katumba alizaliwa Nsabwe wilayani Mukoko na taarifa zinabainisha kuwa, wazazi wake walifariki akiwa na miaka miwili.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka Tume ya Uchaguzi nchini humo, hakuna kijana kama yeye aliyewania urais katika historia ya Uganda ambaye ameweza kugombea baada ya mabadiliko ya katiba ya mwaka 2018 ambayo yaliondoa kigezo cha umri wa kugombea urais.
Katiba ya Uganda kifungu cha 102b kabla ya mwaka 2018 kiliweka wazi kuwa mgombea urais alipaswa kuwa na umri wa miaka 35 hadi 75.
Katumba ameahidi kujenga viwanja vya ndege vya kisasa, kupunguza ukubwa wa baraza la mawaziri, kupunguza gharama za uendeshaji wa serikali, kuboresha huduma za jamii, kuzalisha ajira kwa vijana na kusimamia uhuru wa kujieleza.