The House of Favourite Newspapers

Kikosi Bora cha Mabingwa Afrika, Zimbwe, Luis Ndani

0

NYOTA wawili wa kikosi cha Simba majina yao yameorodheshwa kwenye kikosi bora cha wiki kwenye mashindano ya Ligi ya Mabingwa Afrika hatua ya makundi baada ya mechi nne kuchezwa.

 

Simba ikiwa kundi A inaongoza kundi hilo na ipo na pointi 10 haijaokota bao kwenye hatua ya makundi jambo ambalo ni rekodi kwa msimu huu wa 2020/21.

 

 

Wachezaji hao wawili ni kiungo Luis Miquissone pamoja beki mzawa Mohamed Hussein, ‘Zimbwe’ ambaye ana bao moja pia kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika huku Luis akiwa ametupia mabao mawili.

 

 

Wengine ni Denis Onyango, Mosa Lebusa na Lebohang Maboe hawa ni kutoka Klabu ya Mamelod Sundowns ambayo imetoa wachezaji watatu. Mouad Haddad, Diogenis Joao, Mehd Benaldida, Yasser Ibrahim,Mohamed Magoyafsha na Hamdou Elhouni.

Leave A Reply