The House of Favourite Newspapers

Kila nimpataye ananiacha solemba, nifanyeje?

Anti Liz, mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 25, nimeanza kujitegemea, naishi Bungoni jijini Dar es Salaam na rafiki yangu ninayefanya naye kazi katika kampuni moja.

Kilichonifanya niombe ushauri wako ni tatizo la kukimbiwa na kila msichana ninayempata baada ya kubaini ‘nimejaaliwa’, mpaka nimeamua kuomba ushauri wako tayari nimekimbiwa na wasichana sita.

Kabla ya kubaini kwamba nimejaaliwa, hunipenda na kunisifia kwamba nipo handsome boy lakini tukikutana tu faragha akishaondoka inakuwa jumla na kukata mawasiliano.

Hata hivyo, mmoja wa wasichana hao nilipomuuliza sababu za kukata mawasiliano kanifahamisha ni  kwa sababu ya kujaaliwa kwangu hivyo hawezi kukabiliana nami. Naomba ushauri wako?

Erasto, Dar.

Erasto, naamini kuwa kujaaliwa kwako siyo kikwazo cha wewe kupata mwenza wa maisha kwani wapo wanaume ambao maumbo yao ni madogo lakini wameoa na kuwa na familia.

Subiri muda utafika na kumpata mtu sahihi mtakayefunga ndoa na kufurahia maisha.

Nikikutana naye faragha huishiwa nguvu!

Anti Liz, mimi ni kijana naishi Ngarenaro Arusha, shughuli zangu ni biashara.

Kilichonifanya niombe ushauri wako ni kwamba nina mpenzi wangu ambaye natarajia kumuoa lakini kuna hali inayomtokea tukiwa faragha inanipa hofu sana.

Ni hivi anti, kila tunapomaliza kukutana faragha huishiwa nguvu kwa muda usiopungua saa moja au zaidi ambapo hushindwa kufanya kitu chochote.

Je, atakuwa na tatizo gani?”

Mashaka, Arusha.

Kaka Mashaka, huyo mpenzi wako atakuwa na tatizo ambalo linahitaji kufanyiwa uchunguzi na daktari bingwa wa magonjwa ya akina mama.

Nakushauri nendeni katika hospitali ya wilaya, mkoa au rufaa iliyo karibu yenu ili akafanyiwe uchunguzi na tiba.

Comments are closed.