Kipyenga Kupulizwa AFCON 2021 Cameroon Leo
LEO saa 1:00 usiku, kipyenga kitapulizwa kuashiria kuanza kwa michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2021).
Muda huo mwenyeji Cameroon atafungua pazia dhidi ya Burkina Faso, mchezo utakaopigwa kwenye Uwanja wa Olembe uliopo Mji wa Yaoundé ambao ndiyo mkubwa katika mashindano hayo ukichukua watazamaji 60,000.
Michuano hii ilikuwa inasubiriwa kwa hamu baada ya mwaka jana kushindwa kufanyika kutokana na janga la corona ambalo bado linaendelea kuitikisa dunia kwa sasa. Hakika yatakuwa mashindano yenye mvuto, kutokana na kusheheni masta kibao kutoka kona mbalimbali za ndani na nje ya Afrika.
Kuna baadhi ya wachezaji katika michuano hii wataangaliwa sana kutokana na ubora wao akiwemo Mohamed Salah,
Riyad Mahrez, Sadio Mane, ebastian Haller, Edouard Mendy, Naby Keita na Emmanue Dennis.
Makala haya yanakuletea baadhi ya namba kuelekea mashindano hayo yaliyopita yaliyofanyika mwaka 2019 nchini Misri.