FAMILIA ya mkazi mmoja wa Keko Magurumbasi Jijini Dar, Noja Yohana imejikuta katika wakati mgumu na kutupiwa vyombo nje baada ya jamaa wa familia hiyo aliyejitambulisha kwa jina la Joashi Kinyamagoa kukopa milioni nne kwenye benki moja hapa jijini na huku akitumia nyumba hiyo kama dhamana kisha kushindwa kurejesha mkopo huo.
Imeelezwa kuwa, Kinyamagoa alikopa pesa hizo na kulipa marejesho kadhaa lakini alishindwa kumaliza deni lote kwa wakati hivyo nyumba hiyo akapigwa mnada na kuuziwa mteja mwingine kwa shilingili milioni saba.
Baada ya nyumba hiyo kununuliwa familia hiyo imelalamikia kitendo cha kutupiwa nje vitu vyao na kutaka kubomolewa nyumba yao wakati na wao wamefungua kesi kupinga nyumba yao kuuzwa.
Aidha, Kinyamagoa akizungumza na www.globalpublishers.co.tz amekiri kuchukulia mkopo kwa nyumba hiyo na baada ya kuchelewesha marejesho ndipo ikapigwa mnada lakini alilalamikia nyumba hiyo kuuzwa haraka bila kumvumilia ajitafute ili akalipe deni hilo.
PICHA: RICHARD BUKOS / GPL
Comments are closed.