KISA LAANA QUEEN DARLEEN AMWANGUKIA BABA’KE
BAADA ya kuwa kwenye mgogoro kwa muda mrefu na baba yake mzazi, Abdul Juma ‘Baba D’, ili kukwepa laana ya mzazi, hatimaye msanii wa Bongo Fleva, Mwanahamisi Abdul ‘Queen Darleen’ ametambua umuhimu wa wazazi na kuamua kumfuata na kumuomba msamaha.
Akizungumza na Ijumaa Wikienda, Baba D alisema ni kweli awali alikuwa na ugomvi mkubwa na Queen Darleen na ikafikia hatua mpaka ya kumtamkia maneno mazito kuwa hata akifa binti yake huyo asimzike ila anamshukuru Mungu kwamba mwanaye huyo ametambua makosa yake na kujirudi.
“Haya ni mambo ya kawaida tu katika familia, ni kweli mimi na Queen Darleen tulikuwa na ugomvi mkubwa mpaka ikafikia hatua nikamtamkia maneno mabaya kwamba ikitokea nimefariki dunia asije kunizika, jambo ambalo si zuri, lakini ameyatambua makosa yake, akaja kuniomba msamaha na mimi nikamsamehe kwa moyo mmoja,” alisema Baba D.
STORI: MEMORISE RICHARD, DAR
Comments are closed.