The House of Favourite Newspapers

Kisa Riyama… Mwana achaniwa nguo!

0

Riyama3.jpgRiyama Ally

NA IMELDA MTEMA

DAR ES SALAAM: Msanii wa filamu anayekuja kwa kasi Bongo, Mwanaheri Ahmed hivi karibuni alikumbwa na dhahama alipokatiza Mtaa wa Kongo, Kariakoo jijini Dar baada ya kuchaniwa dera lake kisa kufananishwa na muigizaji mwenzake, Riyama Ally.

Mwanaheri-A-534Mwanaheri Ahmed

Akizungumza na Amani Mwanaheri alisema kuwa, amekuwa akikutana na sintofahamu kubwa njiani baada ya watu wengi kumfananisha na Riyama hata kabla ya yeye kuingia kwenye uigizaji wa filamu.

“Aisee hivi majuzi watu walichana mkono wangu wa dera wakiwa wananivuta na kuniita Riyama huko

 Kariakoo na hata siyo hivyo tu hata kabla sijaingia kwenye tasnia ya filamu wengi wananifananisha naye,” alisema Mwanaheri anayebamba na filamu yake ya Mwanaheri.

Leave A Reply