The House of Favourite Newspapers

Kisa Sakata la Baa la Njaa, Zitto Atishia Kujivua Ubunge

Zitto-KabweBaada ya kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe kupaza sauti kuhusu hali ya chakula nchini huku akisema kuwa serikali haina chakula cha kutosha, viongozi mbalimbali wa serikali akiwemo Rais, Waziri Mkuu na Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi wameibuka na kusema kuwa si kweli kwamba nchi imekumbwa na njaa.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa juzi na Waziri wa Kilimo, Dkt Charles Tizeba ni kuwa serikali ina akiba ya chakula cha kutosheleza. Pia Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akizungumza juzi  mjini Dodoma aligiza Wakala wa Hifadhi ya Taifa ya Chakula kusambaza chakula nchini ili kudhibiti kupanda kwa bei ya vyakula maeneo mbalimbali.
Jana kupitia ukurasa wake wa Facebook, Mbunge Zitto Kabwe aliandika maneno haya;
“Serikali ya CCM ikinionyesha tani 1.5m za chakula kutoka Hifadhi ya Taifa ya Chakula ambazo inataka kusambaza najiuzulu Ubunge mara moja.
 
Narudia, mpaka Oktoba 2016 kulikuwa na nafaka tani 90,400 tu Hivi kwenye maghala yote ya NFRA.
 
Tunashukuru kuwa Hivi sasa ajenda ya tishio la njaa inapata majawabu na matamko. Ndio wajibu wa vyama vya siasa. Kuibua masuala muhimu kwa nchi yetu.
 
Nimesikia Mwenezi wa CCM ameongea na waandishi Leo. Natarajia ndugu Ado Shaibu atamkaribisha mwenzake ulingoni”- Zitto Kabwe

Comments are closed.