The House of Favourite Newspapers

Kiungo Azam FC Chini ya Uangalizi Mkali

0

MFUNGAJI wa bao la kwanza la mashindano kwa msimu wa 2021/22 ndani ya Azam FC, Ayoub Lyanga, yupo chini ya uangalizi mkali wa jopo la madaktari wa timu hiyo ili kumpa huduma itakayomrejesha uwanjani.

 

Lyanga aliyepachika bao mbele ya Horseed FC katika mchezo wa awali wa Kombe la Shirikisho Afrika wakati Azam ikishinda 3-1, alikwama kuyeyusha dakika 90 baada ya kupata maumivu ya mguu na kutoka dakika ya 81.

 

Akizungumza na Spoti Xtra, Ofisa Habari wa Azam FC, Zakaria Thabit, alisema: “Lyanga hakupata majeraha makubwa ila baada ya mchezo ule kumalizika wachezaji walipewa muda wa mapumziko na wanatarajia kuanza mazoezi leo (Jumatatu) jioni.

 

“Kwa Lyanga kabla ya kuanza mazoezi atafanyiwa uchunguzi na madaktari ambao watatoa taarifa kwamba kama anaweza kuanza mazoezi au la.”

DAVID LIWINDA (SJMC) NA LILIANI CHULA (TUDARCo)

Leave A Reply