The House of Favourite Newspapers

KIWANJA CHA MIL. 97 CHA SANCHI CHAZUA GUMZO

Jane Rimoy ‘Sanchi’

MUDA mfupi mara baada ya kuanika kiwanja anachodai kukinunua kwa shilingi milioni 97 maeneo ya Bunju jijini Dar, mwanamitindo Jane Rimoy ‘Sanchi’ amezua gumzo kwa mashabiki wake mitandaoni. 

Sanchi aliweka picha yake mtandaoni ikimuonesha akiwa amesimama katika kiwanja hicho ambacho aliiambia Star Showbiz ya Uwazi kuwa ni muunganiko wa viwanja viwili na bei yake ni milioni 97.

 

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, mashabiki wengi walizua gumzo kwa kuongelea umbo lake huku wengine wakiwasihi wadada wengine waige mfano.“Kumbe ukiwa na umbile kubwa unalipa, cheki anamiliki kiwanja,” ilisomeka moja ya komenti. Kuna haja ya kupata kiwanja Bunju niwe jirani yako nifaidi kwa macho,” ilisomeka komenti nyingine

STORI: IMELDA MTEMA

Comments are closed.