The House of Favourite Newspapers

Kizza Besigye akamatwa tena Uganda

0

160219053129_kizza_besigye_after_release_640x360_bbc

Kiongozi wa chama cha upinzani cha Forum for Democratic Change (FDC).

Kiongozi wa chama cha upinzani cha Forum for Democratic Change (FDC) nchini Uganda Kizza Besigye amekamatwa tena na maafisa wa polisi. Dr. Besigye amekamatwa alipokuwa akijaribu kuondoka nyumbani kwake.

Rais Yoweri Museveni  leo asubuhi  aliongea  na  BBC na kusema kuwa  serikali yake iliamua kumpa kifungo cha nyumbani  ili kuzuia vurugu baada ya zoezi la kupiga kura na kutangaza matokeo.

Museveni alieleza kuwa walichukua uamuzi huo baada ya kubaini kuwa Dk. Besigye alipanga kutangaza matokeo yake mwenyewe ambayo sio ya kweli na kuhamasisha wafuasi wake kufanya fujo, vitendo ambavyo havikubaliki.

“Walikuwa wanataka kufanya fujo. Kwanza walikuwa wanataka kutangaza matokeo yao wenyewe ya uongo. Pili walitaka kufanya fujo za kuharibu mali,” alisema Museveni.

Kadhalika, Museveni alieleza kuwa serikali yake haina mpango wa kuweka ukomo wa Urais nchini humo kwakuwa tayari Bunge liliona ni vyema kuwa na kipindi kisichokuwa na ukomo. Hata hivyo, alisema kuwa hana mpango wa kufanyia marekebisho katiba ya nchi hiyo ili aendelee kubakia madarakani.

“Hakuna mpango wowote. Hatujazungumzia hilo. Lilikuja kwenye baraza la mawaziri tukasema hapana, hakuna haja ya kuongeza,”Museveni anakaririwa.

Katika hatua nyingine, Museveni ambaye anaiongoza Uganda tangu mwaka 1986, amepinga ripoti za waangalizi zilizodai kuwa uchaguzi huo haukuwa huru na haki.

Alisema kuwa wanaotoa madai hayo kwa madai kuwa nguvu ya jeshi ilitumika zaidi hawaijui siasa ya Uganda kwani wanasiasa wengi hawajakomaa kisiasa hivyo wanaweza kuanzisha fujo muda wowote.

Leave A Reply