The House of Favourite Newspapers

KMC Waanza Kuiwinda Yanga SC

0

KIKOSI cha KMC yenye maskani yake Kinondoni jijini Dar, kimeendelea na mazoezi kujiandaa na mchezo dhidi ya Yanga ambao unatarajiwa kupigwa Aprili 10, kwenye Dimba la Mkapa jijini Dar.

 

KMC imekuwa kwenye kiwango bora msimu huu kwenye Ligi Kuu Bara ikishinda mechi 10 kati ya 24 walizoshuka dimbani ikishika nafasi ya tano kwenye msimamo wa Ligi kuu Bara.

 

Akizungumza na Championi Jumamosi kocha msaidizi wa timu hiyo, Habib Kondo amesema: “Kikosi tayari kimeingia kambini kwa ajili ya maandalizi ya mechi yetu na Yanga na mechi za Kombe la Shirikisho, malengo yetu ni kufanya vizuri kwenye mechi zetu zote zilizosalia ili tuweze kumaliza kwenye nafasi za juu kwenye msimamo wa ligi.

“Ushindani kwenye ligi umeongezeka ukizingatia kila timu inapambana kumaliza kwenye nafasi nzuri hivyo ni lazima tufanye maandalizi ya kutosha ili tuweze kufanya vizuri kwenye kila mechi ikiwemo mechi yetu dhidi ya Yanga.

 

KMC inashika nafasi ya tano kwenye msimamo wa Ligi Kuu Bara ikiwa na pointi 35 baada ya kushuka dimbani kwenye mechi 24 wakishinda mechi 10, sare tano na wamepoteza mechi tisa.

STORI: HUSSEIN MSOLEKA, Dar es Salaam

Leave A Reply