The House of Favourite Newspapers

Kocha Azam Ampa Dube Tuzo ya Kagere

0

KOCHA Msaidizi wa kikosi cha Azam, Vivier Bahati, amefunguka kuwa ana imani kubwa kuwa mshambuliaji wao, Prince Dube anaweza kutamatisha utawala wa misimu miwili wa mshambuliaji wa Simba, Meddie Kagere kwa kutwaa tuzo ya ufungaji bora msimu huu.

 

Dube ambaye Jumatano iliyopita katika mchezo wa hatua ya 16 bora ya Kombe la FA, alifanikiwa kuifungia Azam mabao mawili dhidi ya Polisi Tanzania, ndiye kinara wa chati ya wafungaji kwenye Ligi Kuu Bara ambapo mpaka sasa amefanikiwa kufunga mabao 12, akifuatiwa na Kagere mwenye mabao 11.

 

Kagere ndiye anakamatia tuzo hiyo ambayo ameitwaa kwa misimu miwili mfululizo ambapo katika msimu wa 2018/19 aliweka kambani mabao 23, huku msimu uliopita wa 2019/20 akifanikiwa kumaliza msimu na mabao 22.

 

Akizungumza na Championi Jumatatu, kocha Bahati alisema: “Ni jambo lililo wazi kuwa Dube ni miongoni mwa washambuliaji bora kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara kwa sasa.

 

“Japo kuna baadhi ya upungufu wa ufundi ambao tunaufanyia kazi, ambapo naamini baada ya kurekebisha hayo yatazidi kumfanya awe bora na kuna uwezekano mkubwa akaibuka mfungaji bora msimu huu.”

 

Leave A Reply