The House of Favourite Newspapers
gunners X

Kocha Mpya Yanga Cedric Kaze Apewa Miaka Miwili

0
Mwenyekiti wa Yanga, Mshindo Msolla (kulia) akisani mkataba na  kocha mpya wa Yanga, Cedric Kaze.

UONGOZI  wa klabu ya Young SC leo Oktoba 16, 2020 umemtambulisha rasmi kocha mpya wa timu hiyo, Mrundi, Cedric Kaze na kumpa mkataba wa miaka miwili hadi 2020/22 wenye kipengele cha kuongeza mkataba.

 

Kaimu Katibu Mkuu wa kilabu hiyo, Simon Patrick, amesema kandarasi hiyo inaanza rasmi leo na kinachosubiriwa sasa ni kibali tu cha kufanyia kazi.

Kushoto ni Mshauri Mkuu wa Yanga, Senzo Mazingiza, Msolla na Kaze katika hafla ya kumpokea rasmi kocha huyo.

Kaze baada ya kusaini mkataba huo amesema kitu anachotaka kufanya kwa sasa ni kurejesha ukubwa wa timu hiyo huku akiahidi kuonyesha vitendo zaidi uwanjani kuliko maneno.

Kaimu Katibu Mkuu wa Yanga, Simon Patrick na Kaze.

 

 

Leave A Reply