The House of Favourite Newspapers

Kocha Simba Atamba Kuwapiga Red Arrows Mapema Leo

0

PABLO Franco, Kocha Mkuu wa Simba SC, amesema ana dakika 180 za ushindi mbele ya Red Arrows ya
Zambia ili kutinga hatua
ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika.


Mhispania huyo, leo Jumapili
ana dakika 90 za kuiongoza Simba kuibuka na ushindi dhidi ya Red Arrows kwenye
Uwanja wa Mkapa, Dar, kabla
ya Jumapili ijayo kurudiana Zambia ambapo zitatimia dakika 180 za kuamua hatma ya kucheza makundi.


Pablo ameliambia Spoti Xtra
kuwa, amewaambia wachezaji wake wanachohitaji ni ushindi kwa kuwa wataanzia nyumbani ili wakifika ugenini wakamalize kazi.


“Huu mchezo dhidi ya
Red Arrows ni mgumu na siwezi kusema tuna dakika 90 pekee, hapana, bali ni
dakia 180 za kusaka ushindi
na nimewaambia wachezaji kwamba tunapaswa kuanza kushinda hapa nyumbani ili tukamalize kazi ugenini.


“Ni mchezo wangu wa kwanza
kuwa kwenye benchi la ufundi tena Uwanja wa Mkapa ambao una rekodi nzuri. Niliangalia mchezo uliopita ambapo Simba ilipoteza, kuna jambo nimejifunza.


“Mashabiki wamekuwa
wakipenda kuona matokeo mazuri na hilo ndilo ambalo ninahitaji hasa baada ya kupata
ushindi mzuri kwenye mchezo
wa kwanza wa ligi dhidi ya Ruvu Shooting.


“Haina maana kwamba
mbinu itakuwa ni ileile, hapana, kutakuwa na mabadiliko makubwa kuanzia kwenye kikosi
na namna ambavyo tutacheza
kwani haya ni mashindano mengine kabisa ambayo tunashiriki tofauti na mchezo wetu uliopita,” alisema Pablo.

 

AJIBU, SAKHO, KANOUTE NDANI
Kwenye mazoezi ya juzi Ijumaa
ambayo yalifanyika Uwanja wa Mkapa, nyota wote wa Simba walifanya ikiwa ni pamoja na Sadio Kanoute, Ousmane Sakho na Ibrahim Ajibu.

 

Nahodha wa Simba SC, John Bocco alisema makosa ambayo waliyafanya kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Jwaneng Galaxy na kufungwa 3-1, yamewapa somo kubwa.


“Mchezo uliopita tulipoteza
mbele ya Jwaneng Galaxy ambapo tulikuwa tunahitaji kushinda, makosa ambayo
tuliyafanya tumeyafanyia kazi na
tunahitaji ushindi mbele ya Red Arrows.


“Wachezaji tupo tayari na
tunahitaji kupata ushindi, hivyo mashabiki waendelee kuwa nasi, tunaamini kwamba
mchezo utakuwa mgumu na
ushindani mkubwa kwa kuwa tunawaheshimu wapinzani, tutafanya vizuri,” alisema Bocco.


Kuelekea katika mchezo huo wa
leo, Kocha Pablo huenda akaanza na kikosi hiki; Aishi Manula,
Shomari Kapombe, Mohamed
Hussein, Pascal Wawa, Henock Baka, Jonas Mkude, Rally Bwalya, Bernard Morrison, Hassan Dilunga, Meddie Kagere na Kibu Denis.

 

WAANDISHI: Marco Mzumbe,Lunyamadizo Mlyuka na Hawa Aboubkhari.

MWANDISHI WETU, Dar

Leave A Reply