The House of Favourite Newspapers

Kocha wa Simba Maki Atamba Hana Hofu na Yanga Kuelekea Mchezo wa Ngao ya Jamii

0
                                                Kocha Mkuu wa Simba Zoran Maki

ZORAN Maki, Kocha Mkuu wa Simba ameweka wazi kuwa anaamini kwamba watapata matokeo kwenye mchezo wao dhidi ya Yanga kutokana na maandalizi na hana hofu na mechi hiyo.

 

Maki ambaye ni mrithi wa mikoba ya Pablo Franco aliyefungashiwa virago Mei 31, mwaka huu, kete yake ya kwanza itakuwa dhidi ya Yanga, Agosti 13 kwenye mechi ya Ngao ya Jamii katika Uwanja wa Mkapa, Dar.

 

Akizungumza na Championi Jumamosi, Maki alisema kuwa anatambua kuhusu ratiba ilivyo na mechi kubwa ambazo atakutana nazo ikiwa ni pamoja na mchezo dhidi ya Yanga.

 

“Kikubwa ni kuheshimu kila mchezo, najua kwamba kuna Dabi hilo lipo wazi na hata ambapo nilikuwa kulikuwa na jambo kama hili hivyo sina mashaka na mchezo wetu dhidi ya Yanga kikubwa ni maandalizi mazuri,” alisema Maki.

Leave A Reply