The House of Favourite Newspapers

Kubenea Atinga TFF Kuchukua Fomu Ya Urais – Video

0

Mwandishi na Mmiliki wa Chombo cha Habari Said Kubenea leo amefika katika ofisi za shirikisho la Soka Tanzania TFF kuchukua fomu ya Urais kwaniaba ya Ally Saleh lengo ikiwa ni kuisaidia Zanzibar kupata uanachama wa FIFA.

 

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuchukua fomu kubenea amesema lengo la kuchukua fomu hiyo ni kukuza soka la Tanzania na kuisaidia Zanzibar kuwa na uanachama wa FIFA kutokana na kuonekana kero hiyo ni ya muda mrefu na TFF kuonekana kutoifanyia kazi.

 

Aidha katika upande wa wajumbe shabiki na mwanachama kindakindaki wa yanga Jimmy kindoki amejitokeza kuchukua fomu ya Kuwania nafasi ya mjumbe ndani ya TFF huku malengo yake ni kuondoa malalamiko ya yanayokumba soka la Tanzania.

 

Tangu imetangazwa tarehe rasmi ya kuchukua fomu za KUWANIA nafasi mbalimbali ndani ya Tff wadau mbalimbali wametia Nia na ni pamoja na Wallace karia,Oscar oscar ,Evanse mgeusa ,Zahor haji,Ally Saleh ,Ali mayah na Abbas Tarimba. ⚫️ Kwa UPDATES zote, Download GLOBAL APP: ⚫️ ANDROID:http://bit.ly/38Lluc8 ⚫️ iOS:https://apple.co/38HjiCx

Leave A Reply