The House of Favourite Newspapers

KUFURU! Vee Money na Jux Wamwaga Minoti Harusi ya Shilole

Uchebe na Shilole waati wa harusi yao usiku wa kuamkia leo.

COUPLE ya wakali wa Bongo Fleva, Juma Jux na Vanessa Mdee ‘Vee Money’ usiku wa kuamkia leo wamefanya kufuru baada ya kugawa minoti kwenye harusi, Shilole na Uchebe iliyofanyika Masaki jijini Dar es Salaam.

 

Katika harusi hiyo iliyohudhuriwa na mastaa kibao wakiwemo wa Bongo Fleva na Bongo Movies, Couple ya Jux na Vanessa walipata fursa ya kutoa nasaha na kumpongeza Shilole kwa kufunga ndoa pia wakimpongeza Uchebe kwa kumpata mke aliye bora.

Jux na Vanessa.

Kwa upande wa Jux alisema zawadi kubwa anayoitoa kwa Shilole ni kumsomesha mtoto wake mmoja kwa mwaka mmoja huku Vee Money akisema atamlipia muimbaji huyo kulala katika Hotel ya Nyota Tano ya Kilimanjaro.

Baada ya hapo, Jux alichana pochi na kumkabidhi Vanessa mkwanja ambapo aliwavagaa maharusi na kuanza kuwarushia pesa hizo kama zawadi.

SHUHUDIA TUKIO HILO HAPA

Comments are closed.