The House of Favourite Newspapers

‘Kunguru’ Atamani Uhausigeli Kwa Zari

0

kunguruuMsanii wa filamu Bongo, Brenda Malembeka maarufu kama Kunguru

MAYASA MARIWATA

MSANII wa filamu Bongo, Brenda Malembeka maarufu kama Kunguru, anadai anatamani kuwa msaidizi wa kazi za ndani (house girl) kwa Zarinah Hassan ‘Zari’ ambaye ni mzazi mwenzie na Mbongo Fleva Nasibu Abdul `Diamond Platnumz’ kwa ajili ya kumsaidia kumlea mwanaye, Latifa ‘Tiffah’.

Akipiga stori na gazeti hili, muigizaji huyo alisema anavutiwa na aina ya maisha ya mwanadada huyo kwa kuwa si mtu wa kujikweza kama walivyo mastaa wengi Bongo, pia ni mtu mwenye akili ya maisha, hivyo anaamini akifanikiwa kuwa karibu naye hata kwa kumfanyia kazi za ndani bila malipo, atabadilika kifikra.

“Yule dada nampenda kwa kweli, si mtu wa kujisikia hata kidogo, mambo yake anafanya kiakili, si mtu wa kukurupuka ndiyo mana hata Diamond kaamua kujituliza kwake, niko radhi nikawe mtumishi wake, nitafurahi mno, naamini akili yangu itabadilika kutokana na upeo mkubwa alionao Zari wa kusaka maisha,” alisema Kunguru.

Leave A Reply